Kushuka kwa uchumi nchini Marekani kumeshuhudiwa kati ya mwezi Aprili na Juni, kwa mujibu wa watalaam wa masuala ya uchumi, katika kipindi ambacho nchi hiyo imekuwa ikishuhudiwa idadi kubwa ya maambukizi ya virusi vya Corona.
Mwezi Aprili pekee, zaidi ya ajira Milioni 20 zilipotea nchini humo, baada ya biashara kufunga na watu kusalia nyumbani kutokana na janga la Corona.
Wiki iliyopita pekee, watu Milioni Moja na Laki nne waliripoti kupoteza ajira katika taifa hilo lenye uchumi mkubwa duniani, wakati huu wachambuzi wakibashiri kuwa hali huenda ikawa mbaya zaidi katika siku zijazo kabla ya uchumi kuanza tena kuimarika taratibu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |