Ligi ya Europa leo inafika tamati kwa kuzikutanisha timu za Inter milan ya Italia na Sevilla ya Hispania, mechi inayochezwa katika uwanja wa Rheine Energie wa Cologne nchini Ujerumani. Ligi inamalizika katika mazingira magumu kwani tangu mwezi januari baada ya virusi vya Corona kutokea, katika miezi michache iliyofuata ligi lisimama na hata baada ya kuanza mechi zilichezwa bila watazamaji kuwepo, na kupunguza mvuto wa kombe lenyewe.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |