Timu ya Namungo imesema itahakikisha inatoa kpigo kitakatifu katika mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Simba utakaochezwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha jumapili ijayo. Katibu mkuu wa Namungo Ally Selemani amesema, maandalizi ya mchezo huo yanaendelea vema na wamewasili Arusha hii leo kwa ajili ya pambano hilo. Kwa mara ya mwisho timu hizo zilikutana katika fainali ya Kombe la Shirikisho la Azam, ambapo Simba iliibuka kidedea kwa kuifunga Namungo bao 2 – 1 na kutwaa taji hilo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |