• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Jambojet kuanza safari za moja kwa moja kati ya Mombasa na Kisumu

    (GMT+08:00) 2020-09-01 20:02:31
    Shirika la ndege la Jambojet litaanza safari za moja kwa moja kati ya mji wa Mombasa na Kisumu.

    Tayari shirika hilo la bei nafuu limepata idhini ya kufanya safari hiyo kutoka kwa mamlaka ya kuthibiti usafiri wa anga (KCAA).

    Nauli ya miji hiyo miwili itaanzia dola 89 na kutakuwa na safari Ijumaa na Jumapili.

    Mkuu wa mauzo kwenye shirika hilo Titus Oboogi amesema safari kati ya miji hiyo miwili ni kuitikia mahitaji ya wateja.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako