Haya ni kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Shirika la Huduma za Feri nchini Kenya,Bakari Gowa,ambaye amesema idadi ya abiria kivukoni Likoni imepungua kwa kiasi kikubwa na msongamano unaoshuhudiwa ni wa wale wanaokwenda kusaka tonge.
Alisema wanawake na watoto wanaovuka kivukoni hapo wanaenda kupokea chakula cha msaada kinachotolewa na kampuni ya kutengeza simiti.
Aliongeza kuwa hali ngumu ya maisha imesababisha kuongezeka kwa idadi ya watu wanaoenda kupokea chakula hicho.
Gowa anasema msongamano mkubwa wa watu ulitokana na wenyeji wa Likoni waanoenda kutafuta vibarua kila siku lakini tangu kuzuka kwa janga la corona watu wengi walipoteza ajira kufuatia baadhi ya viwanda kufungwa,ndiposa kusababisha idadi ya watu kivukoni hapo kupungua maradufu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |