Barani Ulaya kuna ligi inavyoendelea, ligi inayoitwa Nations league ambayo timu mbalimbali za taifa zilijitupa uwanjani wikiendi kutafuta nafasi ya kuongoza kwenye makundi yao. UINGERZA ilipata ushindi mwembamba ugenini dhidi ya ICELAND, ushindi ambao kwa kiasi fulani unaweza kuonekana kama ni wa bahati kwani hadi dakika 90 za kawaida, timu hizo zilikuwa bado hazijafungana. Raheem Sterling alifunga goli katika dakika za majeruhi na kuipatia ushindi huo. … WEJERUMANI nao wakiwa ugenini walibanwa mbavu bila kutarajia na timu ya USWISI, na kutoka suluhu ya goli moja kwa moja. Wafaransa pia walibahatika kupata ushindi mwembamba wa goli moja kwa bila, goli lililofungwa na mchezaji Kylian Mbappe. Leo kuna mechi 8 zinaendelea lakini ya kukata na shoka itakuwa ni mechi kati ya UHOLANZI dhidi ya ITALIA.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |