Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Afya Duniani Bw. Tedros Adhanom Ghebreyesus amesema chini ya asilimia 10 ya watu waliothibitishwa kuambukiziwa virusi vya Corona na asilimia 0.2 ya vifo vinavyotokana na virusi hivyo kote duniani ni vijana wenye umri chini ya miaka 20, lakini utafiti zaidi unahitajika kuhusu hatari ya ugonjwa huo na kifo miongoni mwa watoto na vijana. Bw. Tedros pia amesema athari za kiafya za muda mrefu kwa watoto na vijana walioambukizwa virusi vya Corona bado hazijulikani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |