• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kenya: Jambojet yaanza kukodisha ndege

    (GMT+08:00) 2020-09-16 18:42:39

    Shirika la ndege la Jambojet ambalo ni tawi la Kenya Airways limeanza huduma ya kukodisha ndege yake moja ili kukabili athari za kupungua kwa wasafiri kutokana na janga la corona.

    Huduma hiyo itakuwa nchini Kenya na kwenye kanda ya Afrika Mashariki.

    Mkurungezi wa Jambo Jet Karanja Ndegwa amesema wanalenga kufanya safari 5 kwa wiki lakini itategemea pia na mahitaji.

    Amesema huduma hiyo inalenga kampuni au familia zinazotaka kusafiri kwa ndege ya kukodi kwenda maeneo mbali mbali.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako