Naibu msemaji wa polisi wa Kampala Luke Owoyesigire amesema, moto umewaka jana asubuhi mapema kwenye Chuo Kikuu cha Makerere nchini Uganda, na kuteketeza vibaya jengo kuu la chuo hicho. Ameeleza kuwa polisi wanafanya uchunguzi juu ya moto huo ulioanza kuwaka majira ya saa sita usiku na kuteketeza mali na nyaraka. Amesema kikosi cha zimamoto na uokoaji zilifika kwenye eneo la tukio na kufanikiwa kudhibiti moto huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |