Mwenyekiti wa Baraza la Utawala nchini Sudan Abdel Fattah al-Burhan ataelekea Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kwa ziara ya siku mbili juu ya masuala yanayohusiana na Sudan. Wakati huo huo, ujumbe wake wa ngazi ya juu utafanya majadiliano na ujumbe kutoka serikali ya Marekani ambayo tayari iko UAE kuhusu kuiondoa Sudan kwenye orodha ya Marekani ya nchi zinazoungaji mkono makundi ya ugaidi, ili kuunga mkono kipindi cha mpito cha Sudan, na kupunguza deni la Sudan kwa Marekani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |