• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Golikipa wa Azam FC aendelea kuwa na rekodi safi

    (GMT+08:00) 2020-09-29 19:05:33

    Golikipa namba moja wa Azam FC David Kissu ameweka rekodi ya kuwa golikipa pekee kwenye Ligi Kuu Bara kucheza dakika nyingi bila kuruhusu bao baada ya kucheza dakika 360 sawa na mechi nne. Kissu alijiunga na Azam FC, akitokea Gor Mahia ya Kenya alipokipiga kwa mafanikio makubwa akifanikiwa kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu mara mbili kwa sasa amekuwa nguzo muhimu kwenye kikosi cha Azam ambacho hakijapoteza mchezo wowote hadi sasa kwenye Ligi Kuu Bara.

    Kisu amepata rekodi hiyo kwenye mechi dhidi ya Polisi Tanzania, Coastal Union, Mbeya City na Tanzania Prisons ambapo amecheza kwa dakika 90 kwenye mechi zote.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako