Watu elfu 60 wamejitolea kupata chanjo ya COVID-19 iliyotengenezwa na China kwenye awamu ya tatu ya majaribio ya kimatibabu, na hakuna madhara yaliyoripotiwa kutokana na chanjo hiyo.
Chanjo nne zilizotengenezwa na China zimeingia kwenye awamu ya tatu ya majaribio ya kimatibabu. Ofisa wa wizara ya sayansi na teknolojia ya China Bw. Tian Baoguo amesema hadi sasa kumekuwa na maendeleo mazuri na hatua ya mwanzo inaonesha kuwa chanjo hiyo ni salama.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |