• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • • CPC waandaa maonyesho ya mafanikio ya awamu ya kwanza ya Rais Xi ikiwemo kuimarika ushirikiano na nchi za Afrika. 2017-10-23

    WAKATI mkutano wa taifa ya 19 wa Chama cha Kikomunisti (CPC) ukiendelea mjini hapa ,Chama hicho kimefungua maonyesho katika ukumbi mkubwa wa vyumba 10 na kuonyesha mafanikio ya awamu ya kwanza ya utawala wa Rais wa nchi hiyo Xi Jinping ikiwemo mahusiano yaliyopo baadhi ya nchi mbalimbali duniani.

    • Wakazi wa Beijing wafanya juhudi ya kuhifadhi mfereji mkubwa 2017-09-29
    Mfereji wa kaskazini mjini Beijing ni sehemu ya kaskazini ya mfereji mkubwa wa Jinghang unaojulikana duniani. Mfereji mkubwa wa Jinghang ni mfereji uliochimbwa na watu wenye urefu mkubwa zaidi na historia ndefu zaidi duniani, ukiwa na urefu wa kilomita 1794. Mfereji huo umeunganisha mito mitano kutoka upande wa kaskazini hadi kusini, ukiwemo mto Hai, mto Manjano, mto Huai, mto Changjiang na mto Qiantangjiang. Mfereji huo umeshuhudia busara ya wachina kuishi kwa amani na mazingira ya asili katika enzi ya kilimo na kutuachia urithi wa hazina ya utamaduni. Wakazi wa Beijing wamefanya juhudi ya kuhifadhi mfereji huo.
    • Maisha mazuri ya mlinzi wa mazingira ya asili wa eneo la chanzo cha mito mitatu nchini China 2017-09-28
    Bw. Zhaxi Cairen mwenye umri wa miaka 28 ni mfugaji aliyezaliwa na kukua katika eneo la ufugaji la mto wa Tuotuo ambao ni chanzo cha mto wa Changjiang. Mwezi wa Agosti, yeye na walinzi wengine wawili wa mazingira ya asili wamebeba mahitaji ya kila siku ikiwemo hema na chakula kuendesha gari kwa umbali wa kilomita 500 kurudi katika kando ya mto wa Tuotuo, ili kufanya doria katika mbuga yenye baridi ambayo ufugaji umepigwa marufuku katika miaka zaidi ya kumi iliyopita.
    • Mji wa Zhoushan wazingatia uhifadhi wa mazingira wakati unapoendeleza uvuvi
     2017-09-25

    Visiwa Zhoushan kwenye bahari ya Donghai viko kusini mashariki mwa China, ni eneo kubwa zaidi la uvuvi nchini China, na nguzo ya uchumi wa mji wa Zhoushan ni shughuli za uvuvi na utengenezaji wa samaki. Naibu mkurugenzi wa idara ya bahari na shughuli za uvuvi ya Zhoushan Bw. Liu Shunbin, amesema mji huo unatilia maanani sana maendeleo ya uvuvi, kwani kati ya wakazi wake milioni moja, laki nne wanafanya kazi zinazohusiana na uvuvi.

    • Eneo la biashara huria la Shanghai lapata uzoefu mkubwa katika kuendeleza shughuli za biashara nchini China 
     2017-09-22

    Eneo la biashara huria la Shanghai ni eneo la majaribio ya biashara huria nchini China. Rais Xi Jinping alipotembelea eneo hilo mwaka 2014 alisema eneo hilo ni kama shamba kubwa la majaribio, baada ya kupata mavuno mazuri, linapaswa kueneza uzoefu wake kwa mashamba mengine. Katika miaka kadhaa iliyopita, eneo hilo limefanya majaribio na uvumbuzi mwingi, na kukamilisha utaratibu wa hali ya juu kuhusu uwekezaji na biashara ambao unakubaliwa na jumuiya ya kimataifa, pia limeeneza uzoefu wake kwa sehemu nyingine nchini China.

    • Wajenzi watimiza thamani yao kwa kuchangia upandaji wa msitu wa Saihanba 2017-08-09

    Msitu wa Saihanba ulioko umbali wa kilomita 200 kutoka Beijing, ulikuwa jangwa kubwa katika miaka 55 iliyopita, lakini sasa umebadilika na kuwa msitu wenye eneo kubwa zaidi duniani iliyopandwa na watu. Je, ni nani walichangia mabadiliko hayo?

    • Macho ya kulinda msitu 2017-08-09

    Kuzuia ajali ya moto ni muhimu zaidi kati ya kazi za kulinda misitu. Katika msitu wa Saihanba ulioko mkoani Hebei, China, ingawa mitambo ya kisasa kama vile rada ya kugundua moto na kamera za uchunguzi zimewekwa, lakini uchunguzi wa binadamu bado ni muhimu zaidi, na watu wa kuchunguza ajali ya moto wanajulikana kama macho ya kulinda misitu.

    • Muujiza wa kubadilisha jangwa kuwa msitu huko Saihanba 2017-08-07

    Msitu wa Saihanba wenye ukubwa wa hekta elfu 74.7 ulioko kilomita 200 kaskazini mwa mji wa Beijing nchini China, ni msitu mkubwa zaidi duniani uliopandwa na watu. Wafanyakazi wa shamba la msitu huo wametimiza muujiza wa kubadilisha jangwa kuwa msitu katika zaidi ya nusu karne iliyopita.

    • Wakulima wa mkoa wa Xizang wanufaika na utalii wa vijiji 2017-08-04

    Kijiji cha Zhangba mkoani Xizang kiliunda shirikisho la utalii wenye umaalumu wa huko mwezi Oktoba mwaka 2010. Kuanzia wakati ule, kijiji hicho kimeshughulikia utalii unaoshirikisha chakula cha Xizang, nyimbo na ngoma, desturi ya maisha ya huko, michezo na kukaa kwenye nyumba za wakulima. Utalii umeleta faida halisi kwa kijiji hicho, na kutoa mchango mkubwa kwa juhudi za kijiji hicho kuondoa umaskini.

    • Mwanakijiji aanzisha kampuni ya chai kusaidia kuondoa umaskini 2017-07-19
    • Bw. Huang Danian:Mwanasayansi wa China, mzalendo wa kweli 2017-07-13
    Mwanasayansi maarufu wa jiofikizia wa China Bw. Huang Danian alifariki dunia Januari 8 mwaka huu, akiwa na umri wa miaka 58. Katika maisha yake mazima Bw. Huang alijitolea nguvu na akili zote kwenye utafiti wake na kuonesha uzalendo kwa taifa.
    • Mtandao wa reli ya kasi wa Delta ya Mto Zhujiang wanufaisha wakazi 2017-07-05

    Tangu miaka ya hivi karibuni mtandao wa reli ya kasi kwenye sehemu ya Delta ya Mto Zhujiang umekuwa ukikamilishwa siku hadi siku, hii si kama tu imeleta fursa kubwa kwa maendeleo ya huko, bali pia imeleta urahisi wa usafari kwa wakazi wa huko. Serikali ya mkoa wa Guangdong hivi karibuni iliweka lengo la kujenga reli ya kasi kwenye miji yote mkoani humo kabla ya mwaka 2020, kukamilika siku hadi siku kwa mtandao huo hakika kutawanufaisha zaidi wakazi.

    • Vijiji vya mlimani vyaondoa na umaskini kutokana na kilimo cha mitishamba 2017-07-05
    Mji mdogo wa Yangba mjini Longnan mkoani Gansu China una mashamba ya kuvutia, milima na misitu ya kupendeza, na hali ya hewa ya kawaida. Mazingira ya kipekee na hali ya hewa nzuri si kama tu vimewapatia wakazi wa huko raslimali nyingi za asili, bali pia zinafaa kwa kilimo cha mitishamba aina ya Gastrodia Elata.
    • Reli ya Chengdu-Ulaya yaleta urahisi kwa usafirishaji wa bidhaa mjini Chengdu 2017-07-03

    Kwenye mji wa Chengdu mkoani Sichuan, kuna duka moja liitwalo "Rong'ou Hui". Ukiingia kwenye duka hilo, utajiona kama uko kwenye supermarket barani Ulaya, ambapo bidhaa mbalimbali za kutoka Ulaya zinauzwa huko. Lakini ni kwa nini duka hilo linauza bidhaa zote zilizoagizwa kutoka Ulaya?

    • Wasomi na mikakati ya China kumaliza umasikini Afrika 2017-06-20

    AFRIKA yenye idadi ya watu zaidi ya bilioni 1.1 ina rasilimali nyingi za asili zenye thamani kama Mafuta, gesi, madini mbalimbali na vinginevyo lakini inakabiwa na changamoto kubwa ya umasikini. Wasomi wa China na Afrika walikutana mwaka jana nchini China na kuzungumzia sababu za Afrika kukithiri kwa umasikini na mikakati ya kupunguza umasikini. Inakadiliwa kuwa asilimia 75 ya nchi masikini duniani ziko katika bara la Afrika. Hali ya Umasikini:

    • Mafanikio na uzoefu wa China katika kupunguza umaskini 2017-06-20

    "LAZIMA tuondoe umaskini ambao upo katika akili zetu kabla ya kuuondoa ndani ya maeneo tunaotawala, kabla ya kusaidia raia na taifa kutoka kwenye minyororo ya umaskini na kuanza barabara ya mafanikio." Haya ni maneno ya kiongozi wa China Xi Jinping katika kitabu chake maarufu "Kuondokana na Umaskini." Kitabu hiki kinatoa maelezo ya kina kuhusu jinsi yeye alifanikiwa kukabiliana na kushinda vita dhidi ya umaskini kama kiongozi katika Ningde, moja ya sehemu ya Mkoa wa Fujian iliyokuwa na umaskini zaidi katika miaka ya 1980.

    • Mkoa wa Qinghai wazingatia kuboresha maisha ya watu na kuondoa umaskini 2017-06-08

    Mkoa wa Qinghai liko uwanda wa juu magharibi mwa China. Hali ya maendeleo ya mkoa huo inakabiliwa na changamoto nyingi. Asilimia 90 ya watu maskini wanaishi katika eneo la milimani au maeneo yenye ukame. Ni vigumu kuwasaidia watu wa huko kuondokana na umaskini kutokana na maafa mengi, na kuwa na msingi dhaifu wa uchumi.

    • Bw. Luo Junyuan kusaidia watu wa mji wa Jing Gangshan kuondoa umaskini 2017-06-06

    Mji wa Jing Gangshan uko katika eneo la mlima wa Luoxiao ambalo kati ya mkoa wa Jiangxi na Hunan. Ni mji wenye rasilimali nyingi za wanyama, miti na una hali ya hewa nzuri. Lakini kutokana na mji huo kuwa katika eneo la milimani, maendeleo yake yameathiriwa. Eneo hilo lilikuwa eneo la maskini zaidi nchini China kutokana na matatizo ya usafiri, na msingi dhaifu wa uchumi. Fadhili Mpunji na maelezo zaidi kuhusu juhudu za mji huo kuondokana na umaskini.

    • Kijiji cha Maerzhuang chatajirika kutokana na ufugaji wa kondoo 2017-05-25

    Kwenye tafrija ya kuwakaribisha viongozi waliohudhuria mkutano wa kundi la nchi 20 (G20) uliofanyika mwaka jana huko Hangzhou, chakula kimoja cha nyama ya kondoo kilikaribishwa na viongozi wengi. Kondoo hao ni kutoka wilaya ya Yanchi mkoani Ningxia, China. Mwandishi wetu wa habari alipofanya mahojiano kwenye wilaya hiyo, ameona kuwa kondoo wa huko wanafugwa kwenye mashamba yenye mazingira asili, na wakati fulani wanaweza kusikiliza muziki. Hivi sasa wakulima wengi wa huko wametajirika kutokana na ufugaji wa kondoo.

    • Uuzaji wa vifaa vya jukwaani vilivyotengenezwa na kijiji cha Huozhuang mkoani Henan vyanufaika na maendeleo ya mtandao wa Internet 2017-05-22
    "Shehuo" ni shughuli za burudani kwa wachina kusherehekea sikukuu ya mwaka mpya wa jadi wa Kichina, ikiwemo ngoma ya simba, na ngoma ya dragon. Utengenezaji wa vifaa vya jukwaani vya Shehuo katika kijiji cha Huozhuang mkoani Henan nchini China una historia ya miaka zaidi ya 100. Zamani wanakijiji walitengenza vifaa hivi katika karahana ndogo na mauzo ya vifaa hivi yalikabiliwa na changamoto nyingi.
    • Mafanikio yaliyopatikana katika kupunguza umaskini katika miaka ya hivi karibuni nchini China 2017-05-18

    Umaskini ni tatizo kubwa linalokabili dunia nzima. Takwimu zilizotolewa mwaka 2016 na Benki ya Dunia zimeonesha kuwa, hivi sasa duniani kuna watu maskini milioni 700. China ikiwa nchi kubwa zaidi inayoendelea, ingawa idadi ya watu wake maskini imepungua kutoka milioni 82 ya mwaka 2012 hadi milioni 40 ya hivi sasa, lakini lengo la serikali ya China ni kutokomeza kabisa tatizo la umaskini kabla ya mwaka 2020. Ili kutimiza lengo hilo, rais Xi Jinping wa China imeagiza kuchukua hatua halisi zenye ufanisi kuhusu suala hilo.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako