Tanzania: Watanzania wahamasishwa kutembelea vivutio vya utalii
2021-03-01 18:43:00| cri

 

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mary Masanja, ametoa wito kwa watanzania  kuweka utaratibu  wa kutembelea vivutio vya utalii vilivyopo  nchini  na kuacha kuamini vivutio ni kwa ajili ya  wageni kutoka nje.

Wito huo umetolewa leo Alhamisi Februari 25, kwenye  kikao cha pili cha bodi ya barabara mkoa wa Mwanza kwa mwaka wa fedha 2020/2021 kilichofanyika jijini Mwanza ambapo amesisitiza ni vvema kila mtu ahamasike kutembelea vivutio vya utalii ikiwemo mbuga  za  wanyama na hifadhi za taifa. 

Amesema Watanzania wanapaswa kuwa wazalendo kwa kupenda  vivutio vyao na kuvitangaza kwani kuanzia mwaka 1993 kulikuwa na watalii waliokuwa wakiingia  kwenye hifadhi 230,000  na hadi kufikia mwaka 2019 idadi ya watalii iliongezeka na kufikia milioni 1.5 waliofanya utalii kwenye mbuga  mbalimbali zilizopo nchini humo.