Misri inashauri Kenya kuhusu urejesho wa utalii
2021-07-21 07:46:43| CRI

Misri ina wekeza juu ya vyombo vya habari vilivyoimarishwa vya jukwaa ya mtandao ya kijamii na soko ka kidijitali na chanjo ili kufufua utalii ulioathirika na janga la covid 19.

Mwenyekiti wa Mamlaka ya Kukuza Utalii ya Misri Ahmed Youssef amesema idadi ya wageni imeongezeka hadi asilimia 45 ya nambari za kabla ya Covid.

Mkutano ulioshirikishwa na Kenya na Saudi Arabia ulitaka kuchunguza njia za ushirikiano wa baadaye, kugawana maarifa na ushirikiano wa karibu ili kufufua sekta ya utalii ya bara.

Wakati wa mkutano huo, Kenya ilitoa Sh10 milioni, kupitia Mfuko wa Ukuzaji wa Utalii, kwa Kituo cha Kudumisha Utalii na Usimamizi wa Mgogoro katika Chuo Kikuu cha Kenyatta.

Waziri wa Utalii Najib Balala amesema kuwa kiasi hicho kitaongeza uimara wa tasnia ya utalii barani Afrika, hadi mahali panapofaa kutalii.

Kenya pia ilisaini Mkataba na Saudi Arabia, juu ya ushirikiano, katika ukuzaji wa utalii.