中国国际广播电台
Eneo la ardhi
Jamhuri ya Watu wa China
yaani China, iko kwenye sehemu
ya mashariki ya Bara la Asia
na kando ya magharibi ya Bahari
ya Pasifiki. Eneo la nchi
kavu la China ni karibu kilomita
za mraba milioni 9.6, ambayo
ni nchi yenye eneo kubwa zaidi
kwenye Bara la Asia, na ni
nchi kubwa ya tatu duniani
ikizifuata Russia na Canada.
Toka kaskazini hadi kusini,
ardhi ya China inaanzia kwenye
chanzo cha Mto Heilongjiang,
kaskazini ya Mto Mo (digri
53.30 ya latitudo ya kaskazini)
mpaka Zengmu Ansha ya ncha
ya kusini ya Visiwa vya Nasha
(digrii 4 ya latitude ya kaskazini),
umbali kati ya kusini na kaskazini
ni kilomita 5500; toka mashariki
hadi magharibi, ardhi ya China
inaanzia sehemu ya makutano
kati ya Mto Heilong na Mto
Usuri (digrii 135.05 ya longitudo
ya mashariki), mpaka Uwanda
wa juu wa Pamier (digri ya
73.40 ya longitude), umbali
kati ya mashariki na magharibi
ni kilomita 5000.
Mpaka wa nchi kavu ya China
una urefu wa kilomita 22,800,
upande wa mashariki, China
inapakana na Korea ya kaskazini,
upande wa kaskazini inapakana
na Mongolia, upande wa mashariki
inapakana na Russia, upande
wa kaskazini magharibi inapakana
na Kazakstan, Kyrgyzstan na
Tajikstan, upande wa magharibi
na wa kusini magharibi inapakana
na Afgahnistan, Pakistan,
India, Nepal, na Buthan, upande
wa kusini inapakana na Myanmar,
Laos na Vietnam. Na upande
wa mashariki na wa kusini
mashariki China inakabiliana
kwa bahari na Korea ya kusini,
Japan, Philipines, Burnei,
Malaysia na Indonesia.
|