Bendera ya Taifa, Nembo la Taifa, Wimbo la Taifa na Mji Mkuu

中国国际广播电台

Bendera ya Taifa
    Bendera ya Taifa, Nembo la Taifa, Wimbo la Taifa na Mji Mkuu

Bendera ya Taifa: Bendera ya Taifa la Jamhuri ya Watu wa China ni Bendera nyekundu yenye nyota tano za manjano, kiasi cha ulinganifu kati ya urefu na kimo cha bedera hiyo ni 3:2. Bendera ya Taifa ina rangi nyekundu ambayo inamaanisha mapinduzi. Nyota 5 zenye pembe 5 kwenye bendera hiyo ni za rangi ya manjano, na kila ncha ya nyota 4 ndogo zenye pembe 5 inaielekea katikakati ya nyota kubwa, ambayo inaonesha mshikamano mkubwa wa wananchi chini ya uongozi wa Chama cha kikomunisti cha China.

Nembo ya Taifa ya Jamhuri ya Watu wa China

      Nembo ya Taifa ya Jamhuri ya Watu wa China: Nembo ya Taifa ya Jamhuri ya Watu wa China inaonesha Bendera ya Taifa, Uwanja wa Tian An Men, gurudumu lenye meno na mashuke ya ngano na mpunga, ambayo inamaanisha mapambano ya mapinduzi ya demokrasia mpya yaliyofanyika tokea harakati za “tarehe 4 Mei” mwaka 1919 na wananchi wa China pamoja na kuzaliwa kwa China mpya yenye utawala wa kidemokrkasi wa uumma chini ya uongozi wa tabaka la wafayakazi na kwenye msingi wa shirikisho la wafanyakazi na wakulima.

 Wimbo wa Taifa

Wimbo wa Taifa wa Jamhuri ya Watu wa China ni wimbo wa “Songa mbele watu mliojitolea”, ambao ulitungwa mwaka 1935, mtungaji wa maneno ya wimbo huu ni mwandishi maarufu wa tamthiria Bwana Tian Han, muziki wa wimbo huu ulitungwa na Bwana Nie Er ambaye alikuwa mwanzilishi wa harakati za muziki mpya wa China. Wimbo huo ulikuwa wimbo wa kauli mbiu ya filamu ya “Vijana waliokumbwa na mashambulizi”. Filamu hiyo ilieleza kuwa baada ya tukio la “Tarehe 18 Septemba” mwaka 1931, Japan iliposhambulia na kuikalia mikoa mitatu ya kaskazini mashariki ya China, taifa la China lilikuwa katika kipindi cha kufa na kupona, ambapo baadhi ya vijana walijitoa kutoka kwenye hali ya uchungu na mahangaiko wakaenda kwenye medani ya vita kupambana na mashambulizi ya Japan. Kutokana na filamu hiyo, wimbo huu uliimbwa na wachina wa kila sehemu nchini China, ukasifiwa kuwa mbiu wa kutoa mwito wa kujipatia ukombozi wa taifa la China.
Tarehe 27 Septemba mwaka 1949, mkutano wa kwanza wa wajumbe wote wa Baraza la mashauriano ya kisiasa la umma la China ulipitisha azimio kuwa kabla ya kutungwa rasmi kwa wimbo wa taifa wa Jamhuri ya Watu wa China, wimbo wa “Songa mbele watu mliojitolea” uwe wimbo wa taifa. Tarehe 14 Machi, mwaka 2004, Mkutano wa pili wa Halmashauri ya kudumu ya 10 ya Bunge la umma la China ulipitisha mswada wa marekebisho ya katiba ukaamua kuwa wimbo wa Taifa wa Jamhuri ya Watu wa China ni wimbo wa “Songa mbele watu mliojitolea ”.

Wimbo wa Taifa

Nyanyukeni!

Enyi msiokubali kuwa watumwa!

Tujenge ukuta mkuu mpya kwa damu na miili yetu!

Taifa la China limekuwa hatarini kabisa,

Kila mmoja analazimika kupaaza sauti ya mwisho.

Nyanyukeni, nyanyukeni, nyanyukeni!

Sote tuwe na nia moja,

Tusonge mbele bila kujali risasi na mizinga!

Tusonge mbele bila kujali risasi na mizinga!

Mbele! mbele! mbele!


Mji Mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China

Mji mkuu wa Jamhuri ya Watu wa China ni Beijing.

Tarehe mosi Oktoba mwaka 1949 mwenyekiti Mao Zedong kwenye roshani ya Tian An Men alitangaza dunia nzima kuwa serikali kuu ya Jamhuri ya Watu wa China imeasisiwa! Tokea hapo, Beijing ukiwa mji mkuu pamoja na China mpya umefungua ukurasa mpya wa historia.