Mamlaka ya Bahari na visiwa
中国国际广播电台


Mwambao wa nchi kavu ya China unaanzia mlango wa Mto Yalu wa Mkoa wa Liaoning wa kaskazini hadi Mlango wa Mto Beilun wa Mkoa wa Guangxi wa kusini, urefu wake ni kilomita 1,800. Hali ya kijiografia ya pwani za bahari ni tambarare, ambapo kuna bandari na ghuba nyingi zenye hali bora, na nyingi ni bandari ambazo maji yake hayawezi kuganda kwa mwaka mzima. Kuna bahari kubwa 5 za karibu nchini China kama vile Bahari ya Bo, Bahari ya Huang, Bahari ya Mashariki, Bahari ya Kusini pamoja na Sehemu ya Bahari ya Pasifiki ya mashariki ya Taiwan. Miongoni mwa hizo, Bahari ya Bo ni bahari ya ndani ya China. Sehemu ya Bahari ya Pasifiki ya mashariki ya Taiwan inaanzia Visiwa vya Xiandao vya kaskazini vilivyoko kusini magharibi ya Visiwa vya Ryukyu vya Japan, mpaka kwenye Mlango wa Bahari ya Bashi wa kusini.
Eneo la bahari la China ni pamoja na maji ya ndani na mamlaka ya bahari ya China, eneo lake la jumla ni zaidi ya kilomita 380,000. Maji ya ndani ya China ni eneo la bahari la Jamhuri ya watu wa China toka mstari wa mamlaka ya bahari unaoelekea upande wa nchi kavu hadi mwambao wa bahari. Upana wa mamlaka ya bahari ya China ni nautical maili 12 kuanzia mstari wa bahari.

Kwenye eneo la bahari ya China kuna visiwa zaidi ya 5000, eneo lake la jumla ni kilomita za mraba 80,000, mwambao wa visiwa ni kilomita za mraba 14,000. Miongoni mwao Kisiwa cha Taiwan ni kikubwa zaidi kuliko vingine vyote, eneo lake ni kilomita za mraba 36,000; Kisiwa cha Hainan ni cha pili kwa ukubwa wake, eneo lake ni kilomita za mraba 34,000. Visiwa vya Diaoyu na Visiwa vya Chiwei vilivyoko kwenye bahari ya kaskazini mashariki ya Kisiwa cha Taiwan ni visiwa vilivyoko kwenye sehemu ya mashariki kabisa ya China. Visiwa vya Dongsha, Visiwa vya Xisha, Visiwa vya Zhongshan na Visiwa vya Nasha vilivyoko kusini kabisa ya China vinaitwa kuwa ni visiwa mbalimbali vya Bahari ya Kusini.