Hali ya Jiografia
中国国际广播电台



Hali ya JiografiaChina ni nchi yenye milima mingi, eneo la sehemu za milimani linachukua theluthi mbili ya eneo la jumla la nchi nzima. Sehemu hizo za milimani ni pamoja na ardhi milimani, vilima na nyanda za juu. Katika eneo lote la China ardhi ya milima inachukua 33 %, nyanda za juu 26 %, mabonde 19 %, tambarare 12 % na vilima 10 %.

Katika mamilioni ya miaka kadhaa iliyopita, Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet ulikuwa kama nundu kwenye ardhi duniani, maumbo ya ardhi ya China yakatokana na uwanda huo. Ukiiangalia ardhi ya China kutoka angani, hali ya kijiografia ya China ni kama ngazi inayoelekea mashariki kutoka magharibi, inatelemka hatua kwa hatua. Kutokana na kugongana kati ya ardhi ya India na ardhi ya Ulaya na Asia, Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet ulijitokeza siku hadi siku, mwinuko wake kwenye usawa wa bahari ni zaidi ya mita 4000, hivyo uwanda huo unaitwa kuwa ni “Paa la dunia”, na kuwa ngazi ya kwanza kwenye ardhi ya China. Kilele kikuu cha Jomolangma cha Mlima Himalaya kwenye Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet kina urefu wa mita 8848.13, ambacho ni kilele cha juu cha kwanza duniani. Ngazi ya pili inaundwa na Uwanda wa Juu wa Mongolia ya ndani, Uwanda wa juu wa Huangtu, Uwanda wa Juu wa Yungui pamoja na Bonde la Talimu, Bonde la Zhungeer na Bonde la Sichuan, wastani wa mwinuko wake kutoka usawa wa bahari ni mita 1000-2000. Ukipita ukingo wa mashariki wa ngazi ya pili ni ngazi ya tatu inayoundwa na Milima Daxinganling, Milima Taihan, Mlima Wu na Mlima Xuefeng inayoelekea pwani ya mashariki ya bahari ya Pasifiki. Katika sehemu ya mwinuko unaotelemka chini ya mita 500 hadi 1000, kuna Tambarare ya Kaskazini ya mashariki, Tambarare ya Kaskazini, na Tambarare ya eneo la katikati na chini ya mtitiriko wa Mto Changjiang, na katika sehemu ya ukingoni mwa tambarare hizo kuna milima mifupi na vilima. Mashariki ya sehemu hiyo ni sehemu inayoelekea kwenye bahari ya China yaani ngazi ya nne, ambapo kimo cha maji ya sehemu kubwa ni chini ya mita 200.