中国国际广播电台
Milima mingi mikubwa na mirefu
imekuwa kama “mifupa” ya ardhi
ya China, na kuundwa kuwa
mifumo mingi tofauti ya milima.
Milima mikubwa maarufu ya
China ni: Milima Himalaya,
Milima Kunlun, Milima Tiansha,
Milima Tanggula, Milima Qinling,
Milima Daxinganling, Milima
Taihang, Milima Qilian, na
Milima Hengduan.
Milima
Himalaya: Milima hiyo wa umbo
wa upinde unatambaa kwenye
sehemu ya mipaka kati ya China
na India na Nepal, urefu wake
ni zaidi ya kilomita 2400,
mwinuko wake kutoka usawa
wa bahari ni mita 6000, ambayo
ni milima mikubwa na mirefu
zaidi kuliko mingine yote
duniani. Mwinuko wa kilele
chake kikuu Jomolangma kutoka
usawa wa bahari ni mita 8848.13,
kilele hicho ni cha juu zaidi
kuliko vingine vyote duniani.
Milima Kunlun: Milima hiyo
inaanzia Uwanda wa juu wa
Pamil katika upande wa magharibi,
na upande wake wa mashariki
unafikia kaskazini magharibi
ya Mkoa wa Sichuan, China,
urefu wake ni zaidi ya kilomita
2500, wastani wa mwinuko kutoka
usawa wa bahari ni mita 5000-7000,
kilele chake cha juu zaidi
cha Gonggeer kina mwinuko
wa mita 7719 kutoka usawa
wa bahari.
Milima Tianshan: Milima Tianshan
inasimama kwenye sehemu ya
katikati ya Mkoa unaojiendesha
wa Xinjiang Uygur wa kaskazini
magharibi ya China, wastani
wa mwinuko wake kutoka usawa
wa bahari ni mita 3000-5000,
kilele chake cha juu zaidi
Tomoer kina mwinuko wa mita
7455.3 kutoka usawa wa bahari.
Milima Tanggula: Milima hiyo
iko kwenye sehemu ya katikati
ya Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet,
wastani wa mwinuko kutoka
usawa wa bahari ni mita 6000,
kilele chake cha juu zaidi
Geladandong kina mwinuko wa
mita 6621 kutoka usawa wa
bahari, ambapo ni chanzo cha
Mto Changjiang ambao ni mto
mrefu zaidi nchini China.
Milima Qinling: Upande wa
magharibi wa milima hiyo inaanzia
mashariki ya Mkoa wa Gansu,
upande wake wa mashariki kufika
sehemu ya magharibi ya Mkoa
wa Henan, wastani wa mwinuko
wake ni mita 2000-3000 kutoka
usawa wa bahari, kilele chake
kikuu Taibai kina mwinuko
wa mita 3767 kutoka usawa
wa bahari. Milima hiyo ni
mstari muhimu wa kijiografia
kati ya kusini na kaskazini
nchini China.
Milima Daxinganling: Upande
wake wa kaskazini unaanzia
sehemu iliyo karibu na Mto
Mo wa mkoa wa Heilongjiang,
kaskazini mashariki ya China,
upande wake wa kusini unafika
eneo la juu la Mto Laoha,
umbali kutoka kusini hadi
kaskazini ni kilomita 1000,
wastani wa mwinuko wa kutoka
usawa wa bahari ni mita 1500,
kilele chake kikuu Huanggangliang
kina mwinuko wa mita 2029
kutoka usawa wa bahari.
Milima Taihang: Toka kaskazini
hadi kusini milima hiyo inatambaa
kwenye ukingo wa mashariki
ya Uwanda wa Juu wa Huangtu,
urefu wake ni zaidi ya kilomita
400, wastani wa mwinuko kutoka
usawa wa bahari ni mita 1500-2000,
kilele chake cha juu zaidi
Xiaowutaishan kina mwinuko
wa mita 2882 kutoka usawa
wa bahari.
Milima Qilian: Milima hiyo
inatambaa katika sehemu ya
ukingoni mwa kaskazini mashariki
ya Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet,
wastani wa mwinuko wa kutoka
usawa wa bahari ni zaidi ya
mita 4000, na kilele chake
kikuu kina mwinuko wa mita
5547 kutoka usawa wa bahari.
Milima Hengduan: Milima hiyo
iko kwenye sehemu ya kusini
mashariki ya Uwanda wa Juu
wa Qinghai-Tibet na katika
sehemu ya makutano kati ya
mipaka ya mikoa mitatu ya
Tibet, Sichuan na Yunnan,
wastani wa mwinuko kutoka
usawa wa bahari ni mita 2000-6000,
kilele chake kikuu Gongga
kina mwinuko wa mita 7556.
Milima Taiwan: Milima hiyo
inapita upande wa mashariki
ya Kisiwa cha Taiwan , wastani
wa mwinuko wake kutoka usawa
wa bahari ni mita 3000-3500,
kilele chake kikuu Yushan
kina mwinuko wa mita 3952
kutoka usawa wa bahari.
Zaidi ya hayo, nchini China
pia kuna milima mingine maarufu
kama vile Mlima Huang, Mlima
Tai, Mlima Hua, Mlima Song,
Mlima Heng, Mlima Ermei, Mlima
Lu, Mlima Wudang na Mlima
Yandang.
|