Milima
中国国际广播电台


       Milima mingi mikubwa na mirefu imekuwa kama “mifupa” ya ardhi ya China, na kuundwa kuwa mifumo mingi tofauti ya milima. Milima mikubwa maarufu ya China ni: Milima Himalaya, Milima Kunlun, Milima Tiansha, Milima Tanggula, Milima Qinling, Milima Daxinganling, Milima Taihang, Milima Qilian, na Milima Hengduan.

      Milima Himalaya: Milima hiyo wa umbo wa upinde unatambaa kwenye sehemu ya mipaka kati ya China na India na Nepal, urefu wake ni zaidi ya kilomita 2400, mwinuko wake kutoka usawa wa bahari ni mita 6000, ambayo ni milima mikubwa na mirefu zaidi kuliko mingine yote duniani. Mwinuko wa kilele chake kikuu Jomolangma kutoka usawa wa bahari ni mita 8848.13, kilele hicho ni cha juu zaidi kuliko vingine vyote duniani.

Milima Kunlun: Milima hiyo inaanzia Uwanda wa juu wa Pamil katika upande wa magharibi, na upande wake wa mashariki unafikia kaskazini magharibi ya Mkoa wa Sichuan, China, urefu wake ni zaidi ya kilomita 2500, wastani wa mwinuko kutoka usawa wa bahari ni mita 5000-7000, kilele chake cha juu zaidi cha Gonggeer kina mwinuko wa mita 7719 kutoka usawa wa bahari.

Milima Tianshan: Milima Tianshan inasimama kwenye sehemu ya katikati ya Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Uygur wa kaskazini magharibi ya China, wastani wa mwinuko wake kutoka usawa wa bahari ni mita 3000-5000, kilele chake cha juu zaidi Tomoer kina mwinuko wa mita 7455.3 kutoka usawa wa bahari.

Milima Tanggula: Milima hiyo iko kwenye sehemu ya katikati ya Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet, wastani wa mwinuko kutoka usawa wa bahari ni mita 6000, kilele chake cha juu zaidi Geladandong kina mwinuko wa mita 6621 kutoka usawa wa bahari, ambapo ni chanzo cha Mto Changjiang ambao ni mto mrefu zaidi nchini China.

Milima Qinling: Upande wa magharibi wa milima hiyo inaanzia mashariki ya Mkoa wa Gansu, upande wake wa mashariki kufika sehemu ya magharibi ya Mkoa wa Henan, wastani wa mwinuko wake ni mita 2000-3000 kutoka usawa wa bahari, kilele chake kikuu Taibai kina mwinuko wa mita 3767 kutoka usawa wa bahari. Milima hiyo ni mstari muhimu wa kijiografia kati ya kusini na kaskazini nchini China.

Milima Daxinganling: Upande wake wa kaskazini unaanzia sehemu iliyo karibu na Mto Mo wa mkoa wa Heilongjiang, kaskazini mashariki ya China, upande wake wa kusini unafika eneo la juu la Mto Laoha, umbali kutoka kusini hadi kaskazini ni kilomita 1000, wastani wa mwinuko wa kutoka usawa wa bahari ni mita 1500, kilele chake kikuu Huanggangliang kina mwinuko wa mita 2029 kutoka usawa wa bahari.

Milima Taihang: Toka kaskazini hadi kusini milima hiyo inatambaa kwenye ukingo wa mashariki ya Uwanda wa Juu wa Huangtu, urefu wake ni zaidi ya kilomita 400, wastani wa mwinuko kutoka usawa wa bahari ni mita 1500-2000, kilele chake cha juu zaidi Xiaowutaishan kina mwinuko wa mita 2882 kutoka usawa wa bahari.

Milima Qilian: Milima hiyo inatambaa katika sehemu ya ukingoni mwa kaskazini mashariki ya Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet, wastani wa mwinuko wa kutoka usawa wa bahari ni zaidi ya mita 4000, na kilele chake kikuu kina mwinuko wa mita 5547 kutoka usawa wa bahari.

Milima Hengduan: Milima hiyo iko kwenye sehemu ya kusini mashariki ya Uwanda wa Juu wa Qinghai-Tibet na katika sehemu ya makutano kati ya mipaka ya mikoa mitatu ya Tibet, Sichuan na Yunnan, wastani wa mwinuko kutoka usawa wa bahari ni mita 2000-6000, kilele chake kikuu Gongga kina mwinuko wa mita 7556.

Milima Taiwan: Milima hiyo inapita upande wa mashariki ya Kisiwa cha Taiwan , wastani wa mwinuko wake kutoka usawa wa bahari ni mita 3000-3500, kilele chake kikuu Yushan kina mwinuko wa mita 3952 kutoka usawa wa bahari.

Zaidi ya hayo, nchini China pia kuna milima mingine maarufu kama vile Mlima Huang, Mlima Tai, Mlima Hua, Mlima Song, Mlima Heng, Mlima Ermei, Mlima Lu, Mlima Wudang na Mlima Yandang.