Mito
中国国际广播电台


      Nchini China kuna mito mingi, miongoni mwao mito zaidi ya 1500 ambayo kila mto ni wenye eneo la kilomita za mraba 1000. Mito hiyo inagawanyika katika mito ambayo maji yake yanatiririka na kuingia baharini na mito isiyoingia baharini. Eneo la mito ambayo maji yake yanaingia baharini, linachukua 64 % ya eneo la jumla la nchi kavu ya China. Mto Changjiang, Mto Huanghe, Mto Heilongjiang, Mto Zhujiang, Mto Liaohe, Mto Haihe na Mto Huihe ni mito ambayo maji yake yanatiririka kuelekea mashariki na kuingia kwenye Bahari ya Pasifiki; Mto Yaluzhangbujiang wa Tibet unatiririka kuelekea mashariki na kutoka nje, tena kuelekea kusini na kuingia bahari ya Hindi, ambapo unapita Bonde kubwa la kwanza duniani la Yaluzhangbujiang lenye urefu wa kilomita 504.6, na kimo cha mita 6009; Mto Erqisi wa Xinjiang ni mto ambao maji yake yanatoka nje na kuingia kwenye Bahari ya Arctic. Mito ile ambayo maji yao yanaingia kwenye maziwa au kupotelea kwenye jangwa na sehemu ya maji yenye chumvi, eneo lake linachukua 36 % ya eneo la jumla la eneo la nchi kavu ya China.
Mto Changjiang ni mto mkubwa wa kwanza wa China, urefu wake wa jumla ni kilomita 6300, ambao ni mto wa tatu kwa ukubwa duniani, ukiifuata Mto Nile wa Afrika na Mto Amazon wa Amerika ya kusini. Eneo la juu ya Mto Changjiang linapita milima na mabonde makubwa, ambapo maliasili nyingi ya maji zinalimbikizwa kwenye sehemu hizo. Mto Changjiang pia ni mto wa kimaumbile wa shughuli za uchukuzi toka mashariki hadi magharibi nchini China. Hali ya hewa ya eneo la katikati na chini la Mto Changjiang ni ya joto na unyevunyevu, kuna mvua za kutosha, na ardhi yenye rutuba, ambapo ni sehemu iliyoendelea kiviwanda na kilimo nchini China.
Mto Huanghe ni mto mkubwa wa pili wa China, urefu wa jumla wa mto huo ni kilomita 5464. Kwenye eneo la huo kuna malisho na mbuga na maliasili nyingi za madini, katika historia yake eneo hilo lilikuwa moja ya machimbuko muhimu ya ustaarabu wa zama za kale za China.

Mto Heilongjiang ni mto mkubwa wa kaskazini ya China, urefu wake ni kilomita 4350, miongoni mwake maji ya eneo la mto huo la kilomita 3101 yanapita sehemu za nchini China.

Mto Zhujiang ni mto mkubwa wa kusini ya China, urefu wake ni kilomita 2214.

Mto Talimu wa kusini ya Xinjiang ni mto mrefu kabisa wa China ambao maji yake hayaingii baharini, urefu wake ni kilomita 2179.

Mbali na mito ya kiasili, nchini China pia kuna mfereji mmoja maarufu unaopita kusini na kaskazini. Mfereji huo ulichimbuliwa kwa nguvu za binadamu kuanzia karne ya 5, ambao ulianzia Beijing, kaskazini ya China hadi Hangzhou wa mkoa wa Zhejiang, mashariki ya China, mfereji huo unapitisha mifumo mitano mikubwa ya Mto Haihe, Mto Huanghe, Mto Huaihe, Mto Changjiang na Mto Qiantangjiang, urefu wa mfereji huo ni kilomita 1801, ambao ni mfereji mrefu zaidi kuliko mingine duniani uliochimbuliwa kwa nguvu za binadamu mapema zaidi duniani.