中国国际广播电台
Nchini
China kuna mito mingi, miongoni
mwao mito zaidi ya 1500 ambayo
kila mto ni wenye eneo la
kilomita za mraba 1000. Mito
hiyo inagawanyika katika mito
ambayo maji yake yanatiririka
na kuingia baharini na mito
isiyoingia baharini. Eneo
la mito ambayo maji yake yanaingia
baharini, linachukua 64 %
ya eneo la jumla la nchi kavu
ya China. Mto Changjiang,
Mto Huanghe, Mto Heilongjiang,
Mto Zhujiang, Mto Liaohe,
Mto Haihe na Mto Huihe ni
mito ambayo maji yake yanatiririka
kuelekea mashariki na kuingia
kwenye Bahari ya Pasifiki;
Mto Yaluzhangbujiang wa Tibet
unatiririka kuelekea mashariki
na kutoka nje, tena kuelekea
kusini na kuingia bahari ya
Hindi, ambapo unapita Bonde
kubwa la kwanza duniani la
Yaluzhangbujiang lenye urefu
wa kilomita 504.6, na kimo
cha mita 6009; Mto Erqisi
wa Xinjiang ni mto ambao maji
yake yanatoka nje na kuingia
kwenye Bahari ya Arctic. Mito
ile ambayo maji yao yanaingia
kwenye maziwa au kupotelea
kwenye jangwa na sehemu ya
maji yenye chumvi, eneo lake
linachukua 36 % ya eneo la
jumla la eneo la nchi kavu
ya China.
Mto Changjiang ni mto mkubwa
wa kwanza wa China, urefu
wake wa jumla ni kilomita
6300, ambao ni mto wa tatu
kwa ukubwa duniani, ukiifuata
Mto Nile wa Afrika na Mto
Amazon wa Amerika ya kusini.
Eneo la juu ya Mto Changjiang
linapita milima na mabonde
makubwa, ambapo maliasili
nyingi ya maji zinalimbikizwa
kwenye sehemu hizo. Mto Changjiang
pia ni mto wa kimaumbile wa
shughuli za uchukuzi toka
mashariki hadi magharibi nchini
China. Hali ya hewa ya eneo
la katikati na chini la Mto
Changjiang ni ya joto na unyevunyevu,
kuna mvua za kutosha, na ardhi
yenye rutuba, ambapo ni sehemu
iliyoendelea kiviwanda na
kilimo nchini China.
Mto Huanghe ni mto mkubwa
wa pili wa China, urefu wa
jumla wa mto huo ni kilomita
5464. Kwenye eneo la huo kuna
malisho na mbuga na maliasili
nyingi za madini, katika historia
yake eneo hilo lilikuwa moja
ya machimbuko muhimu ya ustaarabu
wa zama za kale za China.
Mto Heilongjiang ni mto mkubwa
wa kaskazini ya China, urefu
wake ni kilomita 4350, miongoni
mwake maji ya eneo la mto
huo la kilomita 3101 yanapita
sehemu za nchini China.
Mto Zhujiang ni mto mkubwa
wa kusini ya China, urefu
wake ni kilomita 2214.
Mto Talimu wa kusini ya Xinjiang
ni mto mrefu kabisa wa China
ambao maji yake hayaingii
baharini, urefu wake ni kilomita
2179.
Mbali na mito ya kiasili,
nchini China pia kuna mfereji
mmoja maarufu unaopita kusini
na kaskazini. Mfereji huo
ulichimbuliwa kwa nguvu za
binadamu kuanzia karne ya
5, ambao ulianzia Beijing,
kaskazini ya China hadi Hangzhou
wa mkoa wa Zhejiang, mashariki
ya China, mfereji huo unapitisha
mifumo mitano mikubwa ya Mto
Haihe, Mto Huanghe, Mto Huaihe,
Mto Changjiang na Mto Qiantangjiang,
urefu wa mfereji huo ni kilomita
1801, ambao ni mfereji mrefu
zaidi kuliko mingine duniani
uliochimbuliwa kwa nguvu za
binadamu mapema zaidi duniani.
|