中国国际广播电台
China ni nchi yenye eneo
kubwa, maliasili ya ardhi
ni ya aina nyingi, ardhi ya
kilimo, misitu, ardhi yenye
majani, jangwa na fukwe, zote
zinapatikana nchini China
kwa maeneo makubwa. Lakini
sehemu kubwa ya ardhi ya China
ni milima, sehemu za tambarare
ni chache, na sehemu ya ardhi
ya kilimo na misitu ni ndogo.
Ardhi ya kilimo inapatikana
zaidi katika tambarare na
mabonde mashariki mwa China,
na sehemu nyingi zaidi yenye
misitu iko katika sehemu ya
kaskazini-mashariki na kusini-magharibi
mwa China, na ardhi kubwa
zaidi zenye majani ziko katika
nyanda za juu na sehemu za
milima.
Ardhi ya kilimo:
Hivi sasa nchini China kuna
hekta milioni 1.27 za ardhi
ya kilimo, tukiigawa China
katika sehemu ya mashariki,
katikati na ya magharibi,
ardhi hiyo ya kilimo katika
sehemu ya katikati inachukua
43.2%, na sehemu za mashariki
na magharibi, kila sehemu
inachukua 28.4, na sehemu
kubwa ya ardhi hiyo iko katika
tambarare ya kaskazini-mashariki,
tambarare ya kaskazini ya
China, tambarare iliyoko katikati
na ya mwisho ya Mto Changjiang,
delta ya Mto Zhujiang na bonde
la Sichuan. Ardhi katika tambarare
ya kaskazini-mashariki ni
ardhi nyeusi yenye rutuba
nyingi, mimea inayolimwa zaidi
katika sehemu hiyo ni ngano,
mahindi, mtama, soya, mkonge
na viazisukari. Ardhi katika
tambarare ya kaskazini ya
China ina rangi ya kahawia,
mimea inayolimwa katika ardhi
hiyo ni ngano, mahindi, uwele,
mtama, pamba na njugunyasa.
Katika tambarare kwenye sehemu
ya katikati na ya mwisho ya
Mto Chanjiang mimea inayopandwa
zaidi ni mpunga, machungwa
na rapa. Na katika bonde la
Sichuan mimea inayolimwa zaidi
ni mpunga, rapa, miwa, chai,
machungwa na mabalungi.
Misitu:
Hivi sasa nchini China kuna
hekta milioni 158.94 za misitu
ambazo ni 16.55% ya eneo lote
la China, kwa hiyo China ni
nchi yenye misitu michache
na ikilinganishwa na kiasi
cha misitu kinachofunika 30.8%
ya ardhi ya dunia kwa wastani
China bado iko mbali. Misitu
ya asili inapatikana zaidi
katika sehemu ya kaskazini-mashariki
na kusini-magharibi mwa China,
na katika tambarare ya mashariki
ya China yaani sehemu yenye
watu wengi na maendeleo ya
kiuchumi, na katika sehemu
kubwa ya kaskazini- magharibi
mwa China misitu ni michache
sana.
Misitu ya China ina aina za
miti karibu 2800, na miti
yenye thamani kubwa ni metasequoia
na ginkgo. Ili kukidhi mahitaji
ya maendeleo ya uchumi, China
imefanya harakati za kupanda
misitu. Hivi sasa misitu iliyopandwa
imekuwa hekta milioni 33.79,
na kuifanya China kuwa nchi
yenye eneo kubwa la misitu
iliyopandwa duniani.
Sehemu kubwa ya misitu ya
kiasili nchini China iko katika
kaskazini-mashariki mwa China,
ikiwa ni pamoja na sehemu
ya mlima Daxinganling, Xiaoxinganling
na mlima Changbai. Sehemu
ya kusini-magharibi ya China
ni sehemu ya pili yenye misitu
mingi. Na sehemu ya kusini-mashariki
ya China ni sehemu ya misitu
iliyopandwa. Licha ya misitu
hiyo, nchini China kuna utando
wa misitu ya hifadhi, mathalan,
kanda za misitu hifadhi iliyoenea
katika China ya kaskazini-mashariki,
kaskazini, na kaskazini-magharibi,
jumla zina kilomita 7000 kwa
urefu na hekta milioni 260
kwa maeneo ambayo ni robo
ya nchi kavu ya China, huu
ni mradi mkubwa kabisa duniani
wa hifadhi ya mazingira.
Ardhi yenye majani:
Kuna hekta milioni 266.06
za ardhi yenye majani ambazo
zinafaa kwa malisho nchini
China, kuna aina za majani
ambazo zinafaa kwa malisho
ya mifugo ya aina mbalimbali
katika majira tofauti. Ardhi
yenye majani ni karibu robo
ya eneo lote la China, na
kuifanya China kuwa nchi yenye
ardhi kubwa yenye majani duniani.
Mbuga za majani ya kiasili
nyingi ziko katika sehemu
ya kaskazini-mashariki mwa
China kuanzia mlima Daxinganling,
mlima Yinshan hadi nyanda
za juu za Qinghai-Tibet. Na
mbuga za majani yaliyopandwa
ziko katika sehemu ya kusini-mashariki
ya China ambapo ziko pamoja
na ardhi ya kilimo na sehemu
za misitu.
Sehemu kubwa ya malisho
iko katika Mkoa wa Mongolia
ya Ndani, mifugo iliyofugwa
huko ni farasi Sanhe na ng’ombe
Sanhe. Katika sehemu ya malisho
mkoani Xinjiang wanafugwa
kondoo wa Xinjiang wenye manyoya
laini, kondoo wa Altai wenye
mkia mnene na farasi wa Yili.
Na katika sehemu ya malisho
mkoani Qinghai waliofugwa
wengi zaidi ni yak, ng’ombe
wenye manyoya marefu, na farasi
maarufu wa Hequ. Katika sehemu
ya malisho mkoani Tibet wanaofungwa
zaidi ni yak.
|