Maliasili ya Madini
中国国际广播电台

 

China ina utajiri mkubwa wa madini, na utajiri huo umethibitishwa kuwa ni 12% ya utajiri wote wa madini duniani, na China ni nchi ya tatu yenye utajiri mkubwa wa madini duniani. Hata hivyo, wastani wa umiliki wa madini wa kila Mchina ni 58% tu ya ule wa duniani, wastani huo wa umiliki wa madini kwa kila Mchina unachukua nafasi ya 53 duniani. Hadi sasa madini aina 171 yamegunduliwa na aina 158 zimethibitishwa utajiri wao (aina za nishati 10, aina za metali nyeusi 5, metali za rangi 41, madini yenye metali thamani 8 na madini yasiyo ya metali 91 na madini ya maji na gesi aina 3). China ni moja ya nchi chache zenye utajiri mkubwa wa madini, aina nyingi za kikamilifu za madini. Kutokana na utajiri uliothibitishwa, aina 25 kati ya aina 45 muhimu zilizopatikana nchini China zinachukua nafasi ya tatu duniani, na kati ya aina hizo 25 madini ya udongo adimu, jasi, vanadium, titanium, tantalum, wolfram, kinywe, shura, barite, magnesite, antimony yanachukua nafasi ya kwanza duniani.

Utapakaaji wa madini nchini China ni kama ifuatavyo: Mafuta na gesi asilia yanapatikana kwa wingi zaidi katika sehemu ya kaskazini-mashariki, kaskazini na kaskazini-magharibi ya China. Makaa ya mawe yanapatikana zaidi katika sehemu ya kaskazini, na kaskazini-magharibi ya China. Madini ya chuma yako zaidi katika sehemu ya kaskazini-mashariki, kaskazini na kusini-magharibi ya China. Madini ya shaba mengi zaidi yako katika sehemu ya kusini-magharibi, kaskazini-magharibi, na mashariki ya China. Madini ya risasi na zinki yanapatikana kote nchini China, na madini ya wolfram, risasi, molybdenum, antimony, na udongo adimu yanapatikana zaidi katika sehemu ya kusini, kaskazini mwa China. Madini ya dhahabu na fedha yanapatikana kote nchini na kisiwani Taiwan. Madini ya phosphorus yanapatikana zaidi katika sehemu ya kusini ya China.

Maliasili ya madini muhimu nchini China ni yafuatayo:
Makaa ya mawe: China inaongoza kwa utajiri wa makaa ya mawe duniani. Makaa ya mawe yamethibitishwa kuwa ni tani bilioni 1000 ambayo mengi zaidi yako katika sehemu ya kaskazini, kaskazini-magharibi na hasa katika mikoa ya Shanxi, Shan’xi na Mongolia ya Ndani.

Mafuta na gesi: Mafuta na gesi zaidi ziko katika sehemu ya kaskazini-magharibi, sehemu ya kaskazini-mashariki, kaskazini na sehemu ya mwambao wa mashariki ndani ya bahari. Hadi kufikia mwishoni mwa mwaka 1998 maeneo 509 ya mafuta na maeneo 163 ya gesi yaligunduliwa nchini China. Utajiri wa mafuta umethibitishwa kuwa ni tani bilioni 18.85 ikiwa ni nafasi ya tisa duniani na gesi mita za ujazo bilioni 1950 ikiwa ni nafasi ya 20 duniani. Na mafuta na gesi yaliyoko China bara ni 73.8% na 78.4% ya utajiri wote wa maliasili hiyo.


Madini ya metali:
Metali nyeusi: China imethibitishwa kuwa na utajiri wa chuma, manganese, vanadium na titanium, na kati ya metali hizo, kiasi cha chuma ni tani bilioni 50, kiasi kikubwa kinapatikana katika mikoa ya Liaoning, Hebei, Shanxi na Sichuan.

Metali zenye rangi:
Metali zenye rangi zilizogunduliwa duniani zote zinaweza kupatikana pia nchini China, na kati ya metali hizo udongo adimu unachukua 80% ya dunia nzima na utajiri wa antimony unachukua 40% duniani na utajiri wa wolfram ni mara nne kuliko utajiri wa metali hiyo katika nchi zote nyingine kwa pamoja.