Maliasili ya nishati za upepo, maji na jua
中国国际广播电台


      
Katika eneo kubwa la China kuna mito mingi ambayo ipo katika sehemu nyingi na maanguko ya maji ni makubwa, kwa hiyo nishati za nguvu za maji ni nyingi. Kutokana na takwimu, nishati za maji ni kilowati milioni 680 na umeme kilowati bilioni 5920 kwa mwaka, uwezekano wa kuzalisha umeme kwa mashine ni kilowati milioni 378 na umeme kilowati bilioni 1920 kwa mwaka, kwa hiyo, siyo tu utajiri wa nishati hiyo peke yake bali pia uwezekano wa kutumika kwa ajili ya kuzalisha umeme vyote vinachukua nafasi ya kwanza duniani.

Nishati ya upepo kwenye mita 10 hewani juu ya ardhi ni kilowati bilioni 3.226. Kwa makadirio, uwezekano wa kutumia nishati hiyo ni kilowati milioni 253, na kwenye bahari iliyo karibu na bara (kima cha maji zaidi ya mita 15) nishati hiyo ni mara tatu kuliko ile ya nchi kavu yaani kilowati milioni 750. Nishati ya upepo ipo zaidi katika sehemu ya kaskazini-magharibi, kaskazini na mashariki ya China na kwenye mwambao na visiwa vya kusini-masharini mwa China. Katika sehemu hizo upepo huwa ni mkubwa katika majira ya baridi na Spring, na katika majira ya joto huwa mdogo. Tabia hiyo inasaidia sana umeme unaozalishwa kwa nguvu za maji katika sehemu hizo, kwa kuwa mvua huwa nyingi katika majira ya joto na chache katika majira ya baridi na Spring, kwa hiyo panafaa kuendeleza uzalishaji wa umeme kwa nguvu za upepo. Mwishoni mwa mwaka 1998, China ilikuwa na vituo karibu 20 vya kuzalisha umeme kwa nguvu za maji, uwezo wa mashine ni kilowati laki 2.236, na hivi sasa nchini China kituo kikubwa kabisa cha kuzalisha umeme kwa nguvu za upepo ambacho pia ni kikubwa barani Asia, ni kituo cha Dabancheng kilichoko mkoani Xinjiang, ambacho mashine zake 111 zina uwezo wa kuzalisha kilowati 300, 500 na 600 za umeme, na jumla ya uwezo wa kuzalisha umeme ni kilowati elfu 57.5. Hivi sasa umeme uliozalishwa kwa nguvu za upepo unachukua sehemu moja kwa elfu moja tu katika uwezo wa jumla wa kuzalisha umeme nchini China, kwa hiyo nafasi yake ya kuendelezwa ni kubwa sana.

Nishati ya jua pia ni kubwa nchini China, kwa mwaka nishati ya mionzi ya jua ni sawa na makaa ya mawe tani milioni 240, na theluthi mbili ya ardhi ya China inapita 6000 megajouli kwa mita moja ya mraba, na katika sehemu ya kaskazini-magharibi ya China na mkoani Tibet hata inafikia 8400 megajouli kwa mita moja ya mraba, na kuwa sehemu yenye nishati kubwa ya jua duniani. Kituo cha kwanza cha kuzalisha umeme kwa nishati ya jua kiko katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, uwezo wake ni wati 560, kilianza kutoa umeme tarehe 11 Oktoba mwaka 1982.