中国国际广播电台
Katika eneo kubwa la China
kuna mito mingi ambayo ipo
katika sehemu nyingi na maanguko
ya maji ni makubwa, kwa hiyo
nishati za nguvu za maji ni
nyingi. Kutokana na takwimu,
nishati za maji ni kilowati
milioni 680 na umeme kilowati
bilioni 5920 kwa mwaka, uwezekano
wa kuzalisha umeme kwa mashine
ni kilowati milioni 378 na
umeme kilowati bilioni 1920
kwa mwaka, kwa hiyo, siyo
tu utajiri wa nishati hiyo
peke yake bali pia uwezekano
wa kutumika kwa ajili ya kuzalisha
umeme vyote vinachukua nafasi
ya kwanza duniani.
Nishati ya upepo kwenye
mita 10 hewani juu ya ardhi
ni kilowati bilioni 3.226.
Kwa makadirio, uwezekano wa
kutumia nishati hiyo ni kilowati
milioni 253, na kwenye bahari
iliyo karibu na bara (kima
cha maji zaidi ya mita 15)
nishati hiyo ni mara tatu
kuliko ile ya nchi kavu yaani
kilowati milioni 750. Nishati
ya upepo ipo zaidi katika
sehemu ya kaskazini-magharibi,
kaskazini na mashariki ya
China na kwenye mwambao na
visiwa vya kusini-masharini
mwa China. Katika sehemu hizo
upepo huwa ni mkubwa katika
majira ya baridi na Spring,
na katika majira ya joto huwa
mdogo. Tabia hiyo inasaidia
sana umeme unaozalishwa kwa
nguvu za maji katika sehemu
hizo, kwa kuwa mvua huwa nyingi
katika majira ya joto na chache
katika majira ya baridi na
Spring, kwa hiyo panafaa kuendeleza
uzalishaji wa umeme kwa nguvu
za upepo. Mwishoni mwa mwaka
1998, China ilikuwa na vituo
karibu 20 vya kuzalisha umeme
kwa nguvu za maji, uwezo wa
mashine ni kilowati laki 2.236,
na hivi sasa nchini China
kituo kikubwa kabisa cha kuzalisha
umeme kwa nguvu za upepo ambacho
pia ni kikubwa barani Asia,
ni kituo cha Dabancheng kilichoko
mkoani Xinjiang, ambacho mashine
zake 111 zina uwezo wa kuzalisha
kilowati 300, 500 na 600 za
umeme, na jumla ya uwezo wa
kuzalisha umeme ni kilowati
elfu 57.5. Hivi sasa umeme
uliozalishwa kwa nguvu za
upepo unachukua sehemu moja
kwa elfu moja tu katika uwezo
wa jumla wa kuzalisha umeme
nchini China, kwa hiyo nafasi
yake ya kuendelezwa ni kubwa
sana.
Nishati ya jua pia ni kubwa
nchini China, kwa mwaka nishati
ya mionzi ya jua ni sawa na
makaa ya mawe tani milioni
240, na theluthi mbili ya
ardhi ya China inapita 6000
megajouli kwa mita moja ya
mraba, na katika sehemu ya
kaskazini-magharibi ya China
na mkoani Tibet hata inafikia
8400 megajouli kwa mita moja
ya mraba, na kuwa sehemu yenye
nishati kubwa ya jua duniani.
Kituo cha kwanza cha kuzalisha
umeme kwa nishati ya jua kiko
katika Mkoa wa Mongolia ya
Ndani, uwezo wake ni wati
560, kilianza kutoa umeme
tarehe 11 Oktoba mwaka 1982.
|