中国国际广播电台
China ni nchi yenye aina nyingi
za wanyama, kuna aina 6266
za wanyama wenye uti wa mgongo,
kati yao aina 500 ziko ardhini,
ndege aina 1258, wanaotambaa
aina 376 na walioko majini
na nchi kavu kwa pamoja aina
284, aina za samaki 3862,
jumla ya wanyama hao ni kiasi
cha moja kwa kumi ya aina
zote duniani. Kuna aina elfu
50 za wanyama wasio na uti
wa mgongo, na aina laki moja
na nusu za wadudu.
Kutokana na takwimu, kuna
kiasi cha aina 476 za wanyama
wenye uti wa mgogo wa nchi
kavu nchini China ambazo ni
kiasi cha 19.42% ya aina zote
duniani. Panda wakubwa ni
wanyama wanaopatikana nchini
China peke yake na wanaweza
kukua hadi kuwa na uzito wa
kilo 135 kila mmoja, chakula
chao ni majani na michipukizi
ya mianzi, hivi sasa kuna
1000 tu, na kuwa alama ya
hifadhi ya wanyama pori duniani.
Kongwani anaweza kukua na
kuwa na urefu wa mita 1.2,
ana manyoya meupe na ngeu
nyekundu kichwani. Katika
Asia ya kusini mashariki ndege
huyo ni dalili njema ya maisha
marefu.
Wanyama wanaopatiakana zaidi
katika sehemu za kaskazini-mashariki,
kaskazini, mkoani Tibet, sehemu
za kusini magharibi, katikati
na kusini za China, kutokana
na mazingira tofauti katika
sehemu hizo aina za wanyama
pia ni nyingi.
|