Upatikanaji wa wanyama
中国国际广播电台


      
China ni nchi yenye aina nyingi za wanyama, kuna aina 6266 za wanyama wenye uti wa mgongo, kati yao aina 500 ziko ardhini, ndege aina 1258, wanaotambaa aina 376 na walioko majini na nchi kavu kwa pamoja aina 284, aina za samaki 3862, jumla ya wanyama hao ni kiasi cha moja kwa kumi ya aina zote duniani. Kuna aina elfu 50 za wanyama wasio na uti wa mgongo, na aina laki moja na nusu za wadudu.

Kutokana na takwimu, kuna kiasi cha aina 476 za wanyama wenye uti wa mgogo wa nchi kavu nchini China ambazo ni kiasi cha 19.42% ya aina zote duniani. Panda wakubwa ni wanyama wanaopatikana nchini China peke yake na wanaweza kukua hadi kuwa na uzito wa kilo 135 kila mmoja, chakula chao ni majani na michipukizi ya mianzi, hivi sasa kuna 1000 tu, na kuwa alama ya hifadhi ya wanyama pori duniani. Kongwani anaweza kukua na kuwa na urefu wa mita 1.2, ana manyoya meupe na ngeu nyekundu kichwani. Katika Asia ya kusini mashariki ndege huyo ni dalili njema ya maisha marefu.

       Wanyama wanaopatiakana zaidi katika sehemu za kaskazini-mashariki, kaskazini, mkoani Tibet, sehemu za kusini magharibi, katikati na kusini za China, kutokana na mazingira tofauti katika sehemu hizo aina za wanyama pia ni nyingi.