Hali ya Leo
中国国际广播电台

 

China ni nchi inayoongoza duniani kwa idadi ya watu, kufikia mwishoni mwaka 2002, idadi ya watu wa China ilikuwa ni bilioni 1.28453 mbali na idadi ya watu wa mikoa ya Hong Kong, Macau na Taiwan. Hii ni wastani wa moja kwa tano ya watu wote duniani. China pia ni nchi yenye watu wengi kwa wastani wa eneo, kwa wastani kuna watu 135 katika kila eneo la kilomita moja. Lakini watu hawapatikani kwa wastani katika kila sehemu bali wengi wanakusanyika katika sehemu ya mashariki, wachache katika sehemu ya magharibi. Katika sehemu ya mashariki kwenye mwambao, kwa wastani kila katika eleo la kilomita moja kuna watu zaidi ya 400, katika sehemu ya katikati kuna watu 200 na katika sehemu ya magharibi katika kila eneo la kilomita moja watu hawafiki 10. Hivi sasa wastani wa kuishi kwa wananchi wa China umeongezeka na kuwa miaka 71.4 ( miaka 69.63 kwa wanaume na 73.33 kwa wanawake), umri huo unazidi wastani wa umri wa kuishi duniani kwa miaka mitano, na unazidi nchi zanazoendelea kwa miaka 7, lakini unapungua kwa miaka mitano ukilinganishwa na nchi zilizoendelea.

        Mwaka 2002 mwendo wa ongezeko la idadi ya watu wa China ulizidi kupungua, mwishoni mwa mwaka huo idadi ya watu ulikuwa bilioni 1.28453. Miongoni mwa watu hao, wakazi wa mijini ni milioni 502.12 ambao ni 39.1% ya watu wote; watu wa sehemu za vijijini walikuwa milioni 782.41 ambao ni 60.9 ya watu wote. Idadi ya wanaume ni milioni 661.15 na wanawake milioni 623.38. Watoto kutoka umri wa miaka sifuri hadi 14 ni 22.4%, wenye umri wa miaka tokea miaka 15 hadi 64 ni 70.3%, wazee wenye zaidi ya umri wa miaka 65 ni 7.3%, idadi ya wazee imefikia milioni milioni 93.77. Watoto waliozaliwa katika mwaka 2002 walikuwa milioni 16.47, ambao ni wastani wa 12.86 kwa 1000 ya watu wote; waliokufa walikuwa milioni 8.21, ambao ni wastani wa watu 6.41 katika 1,000; ongezeko la watu lilikuwa milioni 8.26, ambao ni sawa na watu 6.45 kwa kila watu 1000.