Uzazi wa Mpango
中国国际广播电台

 
Uzazi wa mpango ni sera ya kimsingi ya kitaifa nchini China. Uzazi wa mpango unatekelezwa kwa njia ya muunganisho wa uongozi wa kiserikali na hiari ya umma. Uongozi wa serikali unamaanisha kuwa serikali kuu pamoja na serikali za mitaa zinatoa sera na mpango wa ujumla katika udhibiti wa ongezeko la idadi ya watu, kuinua ubora wa idadi ya watu, kuboresha miundo ya idadi ya watu, na kutoa huduma za afya ya uzazi, kupata uzazi bora na malezi bora. Hiari ya umma inamaanisha kuwa wanaofikia umri wa kupata watoto wapange mimba na kuzaa kwa kuzingatia umri, hali ya afya, kazi na uchumi wa familia chini ya mwongozo wa sera na sheria za kitaifa, na kuchagua njia inayofaa kuepuka uja uzito.
Sera kuhusu uzazi wa mpango zinazotumika sasa nchini China ni kuchelewesha umri wa ndoa na uja uzito, kuzaa kwa watoto wachache na malezi bora; na mume na mke kuzaa mtoto mmoja tu. Katika sehemu za vijijini, mume na mke wakiwa kweli wana shida fulani wanaruhusiwa kuzaa watoto wawili; na katika sehemu za makabila madogo madogo sera ni tofauti kutokana na hali tofauti ya idadi ya watu, maliasili, uchumi, utamaduni na mila, kwamba kwa kawaida mume na mke wanaweza kuzaa watoto wawili na katika sehemu nyingine wanaweza kuzaa watoto watatu, na kabila lenye idadi ndogo sana ya watu wa kabila fulani hawawekewi kikomo cha watoto.

Tokea sera za uzazi wa mpango zianze kutekelezwa, kuchelewesha umri wa kuoa, kuzaa, kuzaa watoto wachache na kutoa kwa malezi bora imekuwa desturi katika jamii. Pamoja na hayo uzazi wa mpango umewawezesha wanawake kujinasua kuzaa mara nyingi na adha za nyumba, hali ya afya ya watoto na mama wazazi pia imekuwa bora zaidi.