Hali ya Xinjiang

中国国际广播电台

      Mkoa unaojiendesha wa kabila la wauigur wa Xingjian kwa ufupi unaitwa Xingjian. Uko katika sehemu ya kaskazini magharibi ya China na katikati ya sehemu ya bara ya Ulaya na Asia, ina eneo la kilomita za mraba zaidi ya milioni 1.66 na ni wa kwanza kwa ukubwa miongoni mwa mikoa ya China. Kwa upande wa magharibi na upande wa kaskazini, unapakana na nchi 8 zikiwa ni pamoja na Mongolia, Shirikisho la Russia, Kazakhstan, Kyrgyzstan, Afghanistan, Pakistan na India, ambapo urefu wa mpaka umezidi kilomita 5,400. Xingjian ni mmoja wa mkoa wa China unaochukua nafasi ya kwanza kwa urefu mkubwa wa mpaka na wingi wa idadi ya forodha nchini China.