Mkoa unaojiendesha wa kabila
la wauigur wa Xingjian kwa ufupi
unaitwa Xingjian. Uko katika
sehemu ya kaskazini magharibi
ya China na katikati ya sehemu
ya bara ya Ulaya na Asia, ina
eneo la kilomita za mraba zaidi
ya milioni 1.66 na ni wa kwanza
kwa ukubwa miongoni mwa mikoa
ya China. Kwa upande wa magharibi
na upande wa kaskazini, unapakana
na nchi 8 zikiwa ni pamoja na
Mongolia, Shirikisho la Russia,
Kazakhstan, Kyrgyzstan, Afghanistan,
Pakistan na India, ambapo urefu
wa mpaka umezidi kilomita 5,400.
Xingjian ni mmoja wa mkoa wa
China unaochukua nafasi ya kwanza
kwa urefu mkubwa wa mpaka na
wingi wa idadi ya forodha nchini
China.