中国国际广播电台
Xinjiang iko katika sehemu ya
ndani ya Asia, kutoka upande
wa kaskazini hadi upande wake
wa kusini kuna milima ya Aertai,
Tian na Kunlun pamoja na mabonde
ya Zhungeer na Tulufan kati
ya milima hiyo. Watu wamezoea
kuiita sehemu ya kusini ya mlima
wa Tian kuwa “Xinjiang ya Kusini”,
na sehemu ya kaskazini ya mlima
wa Tian kuwa “Xinjiang ya Kaskazini”
na kuita mabonde ya Hami na
Tulufan “Xinjiang ya Mashariki”.
Miji na vijiji vya Xinjiang
vyote viko pembezoni mwa mabonde
mawili kama mkufu wa lulu.
Mkoani Xinjiang kuna mto
Talimu, ambao ni wa kwanza
kwa urefu kwenye sehemu ya
ndani ya bara, pamoja na ziwa
la Bositeng lenye maji baridi,
ambalo ni la kwanza kwa ukubwa
kwenye sehemu ya ndani ya
bara na bonde la Tulufan,
ambalo ni la kwanza kwa kuinama
chini kabisa nchini China.
Xinjiang iko kwenye sehemu
yenye ukame na yenye tofauti
kubwa sana kati ya hali joto
ya mchana na usiku, sehemu
ya Aletai ina rekodi kuwa
na hali joto baridi kabisa,
wakati sehemu ya Tulufan inakwenda
kinyume chake kabisa nchini
China.
Theluthi mbili za eneo la
jangwa nchini China ziko mkoani
Xingjian, ambayo eneo la jangwa
la Takelamagan ni kilomita
za mraba elfu 33, ni la kwanza
kwa ukubwa nchini na ni jangwa
la pili kwa ukubwa linalohamahama
duniani. Jangwa la Guerbantonggute
lililoko kwenye bonde la Zhungeer
lina eneo la kilomita za mraba
elfu 48, ambalo ni la pili
kwa ukubwa hapa nchini. Katika
majangwa ya nchini kuna rasilimali
nyingi za mafuta ya asili
ya petroli na gesi asili.
Milima yenye theluji na barafu
mkoani Xingjian imekuwa chimbuko
la maji ya mito. Wastani wa
rasilimali wa mkazi wa Xingjian
unachukua nafasi ya mbele
nchini.
|