Ufuatiliaji wa Historia

中国国际广播电台
 

Kabla ya miaka zaidi ya 2,000 iliyopita, Xinjiang ilikuwa moja ya sehemu ya umoja wa makabila mengi ya China. Mwaka 60 KK, enzi ya Han ilianzisha serikali kwenye eneo la magharibi, ambapo Xinjiang ilisimamiwa moja kwa moja na utawala wa enzi ya Han ya magharibi, na eneo lake lilikuwa pamoja ziwa la Baerkashi na sehemu ya Pamier ya hivi sasa. Katika muda wa miaka zaidi ya 1,000 hapa baadaye, sehemu ya Xinjiang imekuwa ikidumisha uhusiano wa kuwa himaya ya serikali kuu ya China, ambayo vitengo vya utawala vilivyowekwa na serikali kuu vimekuwa vikisimamia shughuli za Xinjiang.

Katika enzi ya Qing, miaka zaidi ya 300 iliyopita, serikali kuu ilimweka jemedari wa Yili kwenye mji wa Huiyuan, sehemu ya Yili, Xinjiang, ambaye alitawala eneo lote la Xinjiang. Mwaka 1884, ulianzishwa mkoa wa Xinjiang, ambapo uhusiano kati yake na mikoa mingine ya China uliimarishwa zaidi.

Mwezi Septemba mwaka 1949, Xinjiang ilipata uhuru kwa njia ya amani. Tarehe 1 mwezi Oktoba mwaka huo huo ilianzishwa Jamhuri ya Watu wa China, ni kama mikoa mingine ya China Xinjiang ilikuwa mkoa unaojiendesha kikabila nchini China.