|
|
|
|
|
|
|
中国国际广播电台
Xinjiang ina mwangaza mwingi
wa jua pamoja na ardhi kubwa.
Wakazi wa huko wameendeleza
kilimo kwenye sehemu zenye maji.
Mazao ya kilimo ya Xinjiang
ni pamoja na ngano, mahindi
na mpunga. Mazao ya kiuchumi
ni pamoja na pamba, mboga za
kutengenezea sukari na maua
ya kutengenezea bia. Kati ya
mazao hayo ya kilimo, uzalishaji
wa pamba unachukua nafasi muhimu
nchini China, tena pamba hiyo
ina nyuzi ndefu, ambazo ubora
wake unalingana na pamba maarufu
za Misri.
Xinjiang pia inajulikana kwa
uzalishaji wa matunda na matikiti
ya aina mbalimbali yakiwemo
zabibu, matikiti ya Hami, matikiti
ya maji, matufaha, mapea, mapichi,
mapera, maaprokoti na matunda
mengine, lakini zabibu na matikiti
ya Hami ni matamu sana. Katika
miaka ya karibuni kilimo cha
Xinjiang kimeendelezwa kuwa
kwa haraka na kuwa sekta kubwa
yenye kazi za uzalishaji na
usindikaji.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|