Mifugo ya Xinjiang

中国国际广播电台

     

Xinjiang ina mifugo ya aina nyingi na ni moja ya sehemu muhimu ya ufugaji. Toka zamani, Xingjian ni sehemu inayozalisha farasi bora na wanyama wengine kama ng’ombe, kondoo, punda ngamia na yak. Uzalishaji wa nyama ya kondoo wa Xinjiang unachukua nafasi ya pili nchini China, idadi ya mifugo ni zaidi ya milioni 40.
Eneo la mbuga ya malisho yenye majani mkoani Xinjiang ni kilomita kiasi cha elfu 570 ikichukua 87% ya maeneo ya kilimo, misitu na malisho ya mifugo. Rasilimali ya malisho yenye majani ni muhimu ya na ya kimsingi kwa uendelezaji wa ufugaji wa mifugo mkoani Xinjiang, ambayo kiasi cha 70% ya mifugo ya Xinjiang inategemea majani yake. Xinjiang ni kituo cha uzalishaji wa aina bora na mpya za mifugo nchini China.