|
|
|
|
|
|
|
中国国际广播电台
Kabila
la wauigur ni moja ya makabila
yaliyokuweko toka zamani za
kale, “uigur” ni jina wanalojiita,
ambalo maana yake ni “umoja”
au muungano”. Kabila la wauigur,
ambalo idadi ya watu inazidi
milioni 7, ni kubwa kwenye sehemu
ya Xinjiang,. Kabila hilo la
watu lina lugha na maandishi
yake.
Mavazi ya jadi ya wauigur ni
kuwa wanaume kwa wanawake na
wazee kwa watoto wote wanapenda
kuvaa makofia ya pembe nne na
yenye nakshi za kutariziwa.
Wanaume wanapenda kuvaa kanzu
na shati ndani yake. Wanawake
wanapenda kuvaa gauni na vizibau
vyeusi nje, kuvaa hereni, bangili,
pete na mikufu, wasichana wanapenda
sana kusuka nywele zenye mikia
mingi. Wakazi wa mijini hivi
sasa wanavaa mavazi ya kisasa.
Watu wa kabila la wauigur wana
adabu kubwa, wanapoona wazee
au marafiki, wanazoea kuweka
mikono yao ya kulia kwenye katikati
ya kifua na kuinama kwa mbele
huku wanawasalimia.
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|