Kabila la wa Tadzhik

中国国际广播电台

      Idadi ya watu wa kabila la watadzhik mkoani Xinjiang imefikia zaidi ya elfu 36, na wengi wao wanaishi kwenye wila inayojiendesha ya Tadzhik. Watu wengi wa kabila hilo ni wafugaji na pia wanafanya shughuli za kilimo. Tangu karne nyingi zilizopita walikuwa wamejenga makazi yao kwenye mabonde yenye urefu wa mita kiasi cha 3,000 juu ya usawa wa bahari, wanapanda mbegu za mazao yanayovumilia baridi katika majira ya Spring, kisha wanaswaga mifugo yao kwenye malisho yenye majani yaliyoko kwenye milima, ikifika majira ya kupukutika majani wanarejea vijijini kuvuna mazao waliyopanda na kukaa nyumbani katika siku za baridi kali, wanaishi hivyo mwaka nenda na mwaka rudi. Mwanaume anapenda kuvaa kanzu ndefu isiyo na ukosi na kufunga mkanda kiunoni, katika siku za baridi anavaa koti refu na kofia ndefu iliyoshonwa kwa ngozi ya kondoo. Wanapenda kula samli na vyakula vilivyotengenezwa kwa maziwa.
Watu wa kabila la watadzhik wanayo lugha na maandishi yao. Wanapocheza ngoma huiga mwewe anavyoruka. Mwewe ni alama ya ushujaa, hivyo watu wa kabila hilo wanaita kabila lao ni la mwewe.