 |
 |
 |
 |
 |
|
 |
中国国际广播电台
Ziwa la Kanasi liko katika wilaya
ya Buerjin iliyoko katika sehemu
ya kaskazini yenye umbali wa
kilomita 150 kutoka mji mkuu
wa wilaya. Ziwa hilo liko ndani
ya msitu mnene kwenye sehemu
ya juu ya mlima likiwa na urefu
wa mita 1374 juu ya usawa wa
bahari, eneo la ziwa hilo ni
kilomita za mraba 45.73 na sehemu
yenye maji mengi zaidi ina kina
cha mita 188.5.
Pembezoni mwa ziwa la Kanasi
ni milima mirefu yenye barafu
na theluji, mandhari yake ya
asili inapendeza sana. Sehemu
hiyo ni ya pekee nchini China
yenye wanyama na mimea ya sehemu
ya Siberia ya Kusini vikiwa
na miti aina karibu 800 ikiwemo
miti adimu ya spruce, fir na
Korean pine, aina 39 za wanyama,
aina 117 za ndege, wanyama wanaotambaa
na kuweza kuishi ndani ya maji
aina 4, aina 7 za samaki na
wadudu aina zaidi ya 300, ambazo
aina nyingi zake ziko katika
sehemu hiyo tu. Sehemu hiyo
ina mandhari nzuri ya mbuga
yenye misitu kati yake, maziwa
mengi na yenye thamani kubwa
ya utalii, hifadhi ya mazingira
ya asili, utafiti wa sayansi,
historia na utamaduni.

|
|
 |
|
|
 |
|
 |
 |
 |
 |
|
|
|
|