Mji wa Kale wa Loulan
中国国际广播电台
 

Mji wa kale wa Loulan uko katika sehemu ya kaskazini magharibi ya Luobubo, kusini mwa Xinjiang, ambao ulikuwa mji muhimu sana kwenye njia ijulikanayo kwa “njia ya hariri” hapo zamani. Hivi sasa mji huo umezungukwa na jangwa na chumvi iliyoganda imara, sehemu hiyo imekuwa pori lenye hatari na kutoonekana watu.
Kutokana na vitabu vya historia, mnamo karne ya 2 kabla ya Kristo, Loulan ilikuwa moja ya sehemu iliyoendelea sana kwenye sehemu ya magharibi ya China. Kitu kinachoshangaza ni kwamba dola hilo, ambalo jina lake lilivuma sana, lilitoweka ghafla baada ya kustawi kwa miaka zaidi ya mia 5 au 6. Mji wa kale wa Loulan ulitoweka namna gani? Toka muda mrefu uliopita, suala hilo jambo hilo lilikuwa suala linalofuatiliwa na watafiti wa mambo ya kale na wanasayansi. Loulan pamekuwa mahali penye siri na ajabu panapovutia watu wanaotaka kuvumbua siri ya maumbile ya asili duniani.
Kutokana na uchunguzi uliofanywa kuhusu mji wa kale wa Loulan, mji huo ulitoweka kwa kufunikwa na jangwa kutokana na chanzo cha kimaumbile na shughuli za binadamu ambazo zilifanya maji ya mto kutiririka kwa kubadilisha njia yake. Kutokana na uchunguzi kuwa mji wa kale wa Loulan ulikuwa na eneo la mita za mraba elfu 120, ambao kuta za mji huo zilitengenezwa kwa udongo, matete (bulrush) na vijiti vya miti. Mto mmoja karibu ulipitia katikati ya mji huo kutoka upande wa kaskazini magharibi hadi upande wa kusini mashariki, lakini vilivyobaki hadi hivi sasa ni mnara wa dini ya kibudha pamoja na majengo yaliyoko karibu na mnara huo. Karibu na mji huo kuna mabaki ya mnara wa kupasha habari wakati wa dharura, maghala ya nafaka na makaburi. Ndani ya makaburi ya mji wa Loulan ilifukuliwa maiti kavu ya “mrenbo wa Loulan” ya kabla ya miaka 3,800 iliyopita. Sasa ndani ya mji wa kale wa Loulan bado kuna mabaki ya vipande vya vyungu vya zamani, maturubai ya sufu, nguo zilizochanika na kuoza za hariri pamoja na pesa za shaba na silaha za kale