Pango lenye Sanamu za Kibudha
中国国际广播电台

      Kwenye “njia ya hariri” ndefu ya kuelekea Xinjiang kuna mabaki ya majengo ya ngome yanayojulikana duniani, malango ya njia, hekalu la pango la mawe, nyumba za wageni, makaburi na minara ya kupasha habari wakati usalama unapotishiwa.
Pango lenye sanamu za kibudhaa elfu moja lililoko Kezier na pango la sanamu za kibudha elfu moja lililoko Baizikelike ni mapango maarufu zaidi kutokana na sanamu na mapicha yaliyochongwa na kuchorwa kwenye kuta za pango la mawe ambazo zimeunganisha utamaduni wa China, India na uajemi na kuonesha hali ya uzalishaji mali na maisha ya wakati wa makabila mbalimbali.
Mapango hayo yalitobolwa toka karne ya 6 hadi karne ya 14 kaskazini mashariki ya mji wa Turufan ingawa baadhi ya sanamu na mapicha kwenye kuta za mapango yameharibiwa, lakini eneo linalohifadhiwa bado limefikia mita za mraba zaidi ya 1,200, ambapo panatambuliwa kuwa ni mahali panapohifadhiwa vizuri zaidi penye sanaa za dini ya kibudha duniani.