Mahali Penye Dini za Aina Nyingi
中国国际广播电台

      Xinjiang ni mahali pekee duniani penye aina nne kubwa za dini ya kibudha, kijing, kimoni na kiislam. Mnamo karne ya kwanza, dini ya kibudha ilienezwa hadi sehemu ya mashariki kwa kufuata njia ya hariri na kufikia sehemu nyingi za China. Dini ya kijing ni dhahebu moja la dini ya kikristu, ambalo liliingia Xinjiang katika karne ya 6. Utafiti uliofanywa kuhusu mambo ya kale unaonesha kuwa dini ya kijing ilienea sana huko Xinjiang, na kuwa moja ya kituo cha dini hiyo, isipokuwa ilianza kufifia baada ya dini ya kiislam kuingia huko hapo baadaye. Katikati ya karne ya 10, dini ya kiislam iliingia Kashi kwa kufuata njia ya hariri, na ilienea sana kwenye sehemu ya Xinjiang kati ya karne ya 16 hadi karne ya 17. Hivi sasa wengi wa watu wa makabila kumi ya Xinjiang ni waumini wa dini ya kiislam.


(图:回族信教群众在清真寺做礼拜)