Hali ya Tibet
中国国际广播电台

     Mkoa wa Tibet ni moja ya mikoa mitano inayojiendesha yenyewe nchini China, kwa ufupi mkoa huo unaitwa kuwa Tibet. Tibet iko katika sehemu ya kusini magharibi ya China ikipakana na nchi za Myanmar, India na Bhutan na Nepal kwenye upande wake wa kusini na upande wa magharibi, urefu wa mpaka unakaribia kilomita 4,000. Eneo la Tibet ni kiasi cha kilomita za mraba milioni 1.22 likichukua 12.8% ya eneo la China.
Wastani wa urefu wa mwinuko mkoani Tibet ni zaidi ya mita 4,000, hivyo inajulikana kwa “Paa la Dunia”. Idadi ya wakazi wa Tibet ni zaidi ya milioni 2.6, kati yake idadi ya watu wa kabila la watibet ni milioni 2.5 ikichukua 96% ya jumla ya idadi ya watu wa Tibet. Tibet ni mkoa wenye idadi ndogo kabisa ya watu nchini China, na pia ni mkoa wa kwanza wenye idadi ndogo ya wakazi kwenye eneo la kilomita za mraba moja, ambalo ni pungufu ya watu wawili kwenye eneo la kilomita moja ya mraba.