中国国际广播电台
Kabla ya kuzaliwa Yesu Kristu,
mababu jadi wa watibet walioishi
kwenye uwanda wa juu wa Qingzang
walikuwa na uhusiano na watu
wa kabila la wahan walioishi
sehemu ya ndani ya China.
Baada ya kupita miaka mingi,
watu wa makabila mbalimbali
walioishi kwenye uwanda wa
juu waliungana na kuwa wa
kabila la watibet.
Hali ya vurugu na ya mfarakano
iliyoendelea kwa miaka zaidi
ya 300 ilimalizika mwanzoni
mwa karne ya 7. Shujaa wa
watibet Songzanganbu alianzisha
rasmi enzi ya Turufan na kufanya
Lahsa kuwa mji mkuu wake,
ambapo walijifunza mafanikio
ya teknolojia ya kisasa ya
uzalishaji mali na siasa na
utamaduni wa enzi ya Tang
na kudumisha uhusiano wa kirafiki
na enzi ya Tang katika mambo
ya siasa, uchumi na utamaduni.
Katikati ya karne ya 13 sehemu
ya Tibet iliingizwa katika
nchi ya China na ilitawaliwa
na serikali kuu pamoja na
kuwepo kwa mabadiliko ya enzi
kadhaa.
Baada ya kuanzishwa enzi ya
Qing utawala kwenye sehemu
ya Tibet uliimarishwa zaidi
na kuwa wa kisheria na kiutaratibu.
Baada ya kuasisiwa kwa Jamhuri
ya Watu wa China mwaka 1949,
serikali kuu iliamua kutekeleza
sera ya kuikomboa Tibet kwa
njia ya amani kutokana na
historia na hali halisi ya
huko. Serikali kuu ya umma
ikifuata matarajio la watu
wa Tibet ilifanya mageuzi
ya demokrasia na kuvunja utaratibu
wa kimwinyi katika Tibet,
tokea hapo watumwa wa huko
walipata uhuru na kutouzwa,
kubadilishwa au kuwa mali
ya matajiri ya kulipia madeni
yao. Mkoa unaojiendesha wa
Tibet ulianzishwa rasmi mwezi
Septemba mwaka 1965.
|