Kabila la watibet ni lenye idadi
kubwa ya watu kwenye sehemu
ya Tibet. Watibet wanashughulikia
zaidi kazi za kilimo na ufugaji,
wakati wakazi wa mijini wanashughulikia
kazi ndogo ndogo za ufundi,
uzalishaji bidhaa viwandani
na biashara.
Watibet ni waumini wa dini ya
kibudhaa ya kitibet. Watu wa
kabila hilo ni wachangamfu na
ni hodari sana kwa uwindaji
na uchezaji ngoma. Watibet wanapenda
kuvaa mashati yenye mikono mirefu;
wanaume wanavaa kanzu kubwa
nje, wanawake wanavaa kanzu
isiyo na mikono na kufunga mkanda
kiunoni, na wanawake walioolewa
wanapenda kuvaa vitambaa vyenye
rangi mbalimbali kama za upinde
wa mvua. Wanaume kwa wanawake
wanapenda kufuga nywele ndefu
na kusuka mikia ya nywele na
kupenda kuvaa mapambo ya hereni,
bangili na pete. Chakula kikuu
cha watu watibet ni unga wa
mseto wa shayiri ya uwanda wa
juu (highland barley) na choroko
na kupenda kunywa chai ya samli
na pombe na kula nyama za ng’ombe
na kondoo.