Kabila la wamenba  
中国国际广播电台

Kabila la wamenba ni kabila la kale kwenye Uwanda wa juu wa Tibet, watu wengi wa kabila hilo wanaishi katika sehemu ya kusini ya Mkoa unaojiendesha wa Tibet. Wamenba wanategemea kazi ya kilimo na ufugaji, uwindaji na kazi ndogo ndogo za mikono. Wamemba wote wanapenda kunywa pombe na kuvuta tumbaku. Wengi wanaamini dini ya kibudha ya kitibet.