VIWANDA
中国国际广播电台

      Hapo zamani Tibet ilikuwa na karakana za ufundi wa jadi wa kutengenezea mazulia, vitambaa vya sufu, apron, viatu, bakuli za mbao na vitu vingine vidogo vidogo. Baada ya Tibet kukombolewa kwa njia ya amani mwaka 1951, hususan baada ya kufanya mageuzi ya demokrasia mwaka 1959, vilijengwa viwanda vingi vya uzalishaji wa umeme, uyeyushaji madini, uchimbaji wa makaa ya mawe, mitambo, kemikali, vifaa vya ujenzi, viwanda vya kazi kuhusu misitu, viberiti, plastiki, nguo, chakula, ngozi na karatasi.
Mwaka 2003, pato la viwanda vya Tibet lilifikia Yuan za Renminbi bilioni 1.8, kiasi hiki kilichukua 15% ya jumla ya pato la Tibet. Katika siku za baadaye Tibet itaendeleza kazi za viwanda, kurekebisha muundo wa uzalishaji mali, na kujitahidi kuendeleza matumizi ya raslimali za aina tatu za madini, misitu na mazao ya mifugo, licha ya hayo itaendeleza mageuzi ya teknolojia ya viwanda na kuongeza pato la viwanda.