Ufugaji
中国国际广播电台

     Ufugaji ni njia muhimu ya uchumi mkoani Tibet, na u na historia ndefu na una nafasi kubwa ya kuendelea zaidi. Hivi sasa kuna mbuga za majani zenye ukubwa karibu hekta milioni 82, kati ya eneo hilo mbuga zinazoweza kutumika kwa ajili ya malisho ni hekta milioni 56, kiasi ambacho moja kwa tano ya malisho yote nchini China na ni moja ya sehemu tano kubwa za ufugaji nchini China.

Ufugaji unachukua 60% ya uchumi wa Tibet, wanyama wanaofungwa ni nyati na kondoo. Wanyama hao ni wa kabila la Tibet, ambao wanasifa ya kuvumilia baridi na ukame.