Mradi wa Kuusaidia Mkoa Tibet
中国国际广播电台

     Mkoa Tibet ambao unajulikana kama ni paa la dunia uko nyuma kiuchumi kutokana na sababu za kihistoria na mazingira ya kimaumbile. Mwaka 1994 serikali kuu ilifanya mazungumzo ya mara ya tatu na inaanzisha mradi wa kuusaidia Mkoa Tibet, mradi huo unahusu, ufugaji, misitu, nishati, mawasiliano, mawasiliano ya posta, jumla unahitaji yuan bilioni 4.86. hivi sasa mradi huo umekamilika na kuanza kutoa mchango mkubwa.

Msaada wa Mkoa Tibet umesaidia kuboresha maisha ya watu wa Tibet. Mjini Lhasa wenyeji wanaweza kuangalia TV, majumba ya ghorofa yamejengwa badala ya zile nyumba za chini za zamani, watoto wa wakulima wanaokwenda shule, bendera za rangi mbalimbali zinapepea mbele ya Kasri la Potala zikiwavutia watalii kwa mwaka mzima.