Kasri la Potala
中国国际广播电台

        Kasri la Potala liko mlimani kaskazini magharibi mwa mji wa Lhasa, ni kasri lililo juu kabisa duniani. Kasri hilo lilijengwa katika karne ya 7, lina ghorofa 13 na eneo la hekta 41. kasri hilo limepakwa rangi ya dhahabu na kutiwa lulu zaidi ya 4000, ni mahali pa dini ya Buddha anapoishi, kufanya kazi na shughuli za kidini.

Mwaka 1961 kasri la Potala iliorodheshwa katika orodha ya urithi wa kitaifa, kila mwaka serikali kuu inatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wake. Tokea mwaka 1989 hadi 1994 serikali kuu ilitenga yuan milioni 5.3 kwa ajili ya ukarabati wake.