Hali ya jumla ya elimu ya Tibet
中国国际广播电台

     China inatekeleza sera ya kutoa elimu bure mkoani Tibet. Gharama za masomo ya wanafunzi toka shule za msingi hadi vyuo vikuu zote zinatolewa na serikali. Sera hiyo nafuu inatekelezwa mkoani Tibet tu. Katika Tibet ya zamani, hakuna shule moja inayomaanisha hali ya zamani tulizo nazo, sembuse chuo kikuu, lakini hivi sasa kuna vyuo vikuu vinne mkoani Tibet.

Ili kusaidia Tibet kuendeleza elimu, tokea mwaka 1985, serikali kuu ya China ilianzisha daraja au shule ya Tibet katika mikoa na miji 21 nchini humo, ambapo wanafunzi elfu 10 hivi wa Tibet wamehitimu kutoka vyuo vikuu au shule za sekondari, na serikali kuu iliwalipia gharama zote za masomo.

Ilipofika mwishoni mwa mwaka 2003, shule za ngazi na aina mbalimbali zipatazo 1011 zilijengwa mkoani Tibet, wanafunzi walifika laki 4.534, na asilimia 91.8 ya watoto wenye umri wa kwenda shule wamesoma shule; watu wasiojua kusoma au kuandika wamepungua na kufikia chini ya asilimia 30. Na tokea mwaka 1992, “shule za matumaini” zaidi ya 180 zilijengwa mkoani Tibet ili kunasaidia watoto wa familia zenye matatizo ya kiuchumi waende shule, ambapo wanafunzi elfu 36 walipata misaada.