Desturi za kidini za Raia wa Tibet
中国国际广播电台

       Watu wa Tibet wana uelewa wa kutosha wa kuamini dini. Watu wengi wa makabila ya watibet, wabenba, waloba na wanaxi wa mkoa unaojiendesha wa Tibet ni waumini wa dini ya kibudha ya kitibet, pia kuna waumini wengi wa dini ya kiislamu na kikatoliki. Hivi sasa mkoani Tibet kuna sehemu zaidi ya 1700 za kufanyika shughuli za dini ya kibudha ya kitibet, watawa wa kiume na kike wanaokaa katika mahekalu wamefikia elfu 46; kuna misikiti minne, waumini wa dini ya kiislamu zaidi ya 3000; kanisa moja ya kikatoliki, waumini zaidi ya 700.

Watu wa kabila la watibet na makabila mengine madogo madogo mkoani Tibet wana haki na uhuru wa kuishi maisha na kufanya shughuli za jamii kwa kufuata desturi na mila zao wenyewe. Wanapodumisha desturi na mila yao ya jadi katika mavazi, chakula na makazi ya makabila yao, pia wamejifunza desturi mpya zinazoonesha ustaarabu wa zama za hivi sasa na maisha mazuri katika malazi na chakula pamoja na shughuli za kufunga ndoa au mazishi. Watu wa mkoa wa Tibet wanaendelea kufanya shughuli nyingi za jadi kama vile za kusherehekea mwaka mpya wa jadi wa Tibet, sikukuu ya mavuno na sikukuu ya Xuedun pamoja na shughuli nyingi za kidini. Pia watibet wa hivi sasa pia wanafanya shughuli mpya za aina mbalimbali za China na ng'ambo.