Tangka
中国国际广播电台

       Tangka ni tamshi la kitibet, nayo ni picha za rangi zilizotariziwa au kuchorwa kwenye vitambaa, hariri au karatasi. Picha hizo ni aina moja yenye mtindo wa utamaduni wa kabla la watibet.

Inasemekana kuwa, katika zama za kale, binti mfalme Wencheng alipoolewa Tibet, alikwenda na ufundi wa kufuma nguo, kutokana na picha hizo tunaweza kuona kuwa ufundi huo wa uzalishaji ulitumiwa na kuenea huko Tibet wakati huo. Rangi zilizotumika katika uchoraji wa picha hizo zilitengenezwa kwa njia ya kisayansi, ndani yake zilitiwa madini na mimea, tena hali ya hewa ya uwanda wa juu wa Tibet ni isiyo na unyevu, hivyo picha za Tangka hata zilichorwa karne kadhaa zilizopita, rangi zake bado zinaonekana ni nzuri za kupendeza kama zilivyo za picha mpya.

    Yaliyochorwa kwenye Tangka yanahusu mambo yote ya maisha ya jamii, hata kama ni histoira ya jamii, na shughuli za kidini zimeoneshwa zaidi katika picha za Tangka.