Tiba za kabila la wahui ni mchanganyiko wa tiba za jadi za kichina na tiba za kiislamu. Katika maendeleo ya miaka mingi, tiba za kabila la wahui zimekuwa na mbinu zake za kipekee, ambazo ni dawa kuchanganywa na chakula. Kwa mfano, wahui wanachanganya mafuta ya ufuta na Glauber's salt kutibu ugonjwa wa kutokuwa na choo ( constipation) .